Home » » Dk Shein afanya uteuzi mpya wa mwenyekiti wa baraza la chuo cha kilimo.

Dk Shein afanya uteuzi mpya wa mwenyekiti wa baraza la chuo cha kilimo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DKT Ali Mohamed Shein  amemteuwa Abdulsalam Issa Khatibu kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha Kilimo, Kizimubani.

Kwa mujibu wa Taarifa kutoka  kwa Mkurugenzi wa Idara ya  Mawasiliano Ikulu Hassan Khatib imeeleza kuwa Abdulsalam  anachukuwa nafasi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza hilo Makame Salum ambaye muda wake wa Kikazi ulimalizika.

Abdulsalam  Issa aliwahi kuwa Mbunge wa CCM  wa Jimbo la Makunduchi na ni Mtaalamu wa mambo ya Kilimo ambaye alifanyakazi ndani na nje ya nchi katika Mashirika yakimataifa.

Aidha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DKT Ali Mohamed Shein amemteuwa Mayasa Salim Ali kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Tiba Asili na Mbadala Zanzibar.

Uteuzi huo umeanza tarehe 27Septemba 2012.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
29/9/2012

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa