Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mhe. Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo, akimfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipowasili nyumbani kwa Rais Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba 2026, kufuatia kifo cha mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia tarehe 07 Septemba 2026 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar.
MTUME MWAMPOSA,MCHUNGAJI KAPO WAMFARIJI RAIS SAMIA KIZIMKAZI ZANZIBAR
Mtume Boniface Mwamposa pamoja na Mchungaji Tony Kapola wakimfariji Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba 2026, kufuatia kifo cha mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia tarehe 07 Septemba 2026 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar.
NAIBU WAZIRI MHE. MHANDISI MARYPRISCA MAHUNDI AMFARIJI RAIS SAMIA
Kizimkazi, Zanzibar | Septemba 8, 2026
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, ambaye pia ni Mbunge anayewakilisha Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Mbeya, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, leo Septemba 8, 2026, amekutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, nyumbani kwake Kizimkazi, Zanzibar, na kumpa pole kufuatia kifo cha Mwenza wake, Mzee Hafidh Ameir Hassan.
Mhe. Maryprisca amemfariji Rais Samia na familia yake kufuatia msiba huo, huku akitoa pole na kuwaombea moyo wa subira, uvumilivu na faraja katika kipindi hiki cha majonzi.
Mzee Hafidh Ameir Hassan alifariki dunia Septemba 7, 2026, wakati alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mzena na amezikwa siku hiyo hiyo Visiwani Zanzibar.



