Home » » POLISI ZANZIBAR YAMDAKA TAPELI KWA KUJIZOLEA MILIONI 6 AKIJIFANYA ANANAFASI YA KAZI YA USALAMA WA TAIFA

POLISI ZANZIBAR YAMDAKA TAPELI KWA KUJIZOLEA MILIONI 6 AKIJIFANYA ANANAFASI YA KAZI YA USALAMA WA TAIFA


Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi ACP Abubakar Khamis Ally akizungumza na Waandishi wa Habari, Ofisini kwake Madema, Zanzibara. 

..........................

Polisi, Zanzibar

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi linamshikilia Marco Daud Zagamba (32) wa Mbweni, kwa tuhuma za kujipatia sh. milioni 6 kwa njia ya utapele wa kuwapatia ajira watu mbalimbali kati Idara ya Usalama wa Taifa na vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Madema, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi ACP Abubakar Khamis Ally amesema mtuhumiwa huyo aliwatapeli wananchi kwa kuwaahidi kuwapatia ajira kwenye Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Idara ya Usalama wa Taifa.

Amefafanua kwamba mtuhumiwa huyo hutumia mbinu ya kujifanya mtumishi wa Serikali na kuwa ana uwezo wa kutoa ajira ambapo alifanya hivyo akijua kuwa ni kinyume cha sheria.

Ametoa mwito kwa wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya watuhumiwa wa utapeli hasa kipindi hiki ambacho Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP. Camillus Wambura ametangaza usaili kwa waombaji wa ajira za Jeshi la Polisi.

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa