na Mauwa Mohammed, Zanzibar
SERIKALI ya
Mapinduzi Zanzibar inakusudia kuanzisha sheria itakayozingatia ubora wa majengo
ambayo yatakuwa rafiki kwa watu wenye ulemavu nchini.
Kauli hiyo
ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati wa Mfuko wa Watu wenye ulemavu, Nassor
Ahmed Mazrui, alipozungumza na waandishi wa habari mjini hapa.
Alisema kamati
na baraza la watu wenye ulemavu litaandaa sheria ndogondogo, ili majengo yote
yatakayojengwa na serikali na watu binafsi yazingatie mahitaji ya watu wenye
ulemavu.
Mbali na hilo,
alisema kamati hiyo itaandaa harambe ya kuchangia mfuko wa watu wenye ulemavu
Septemba 28 mwaka huu, ili kuondoa changamoto zinazowakabili watu hao.
Alisema mfuko
huo utawasaidia watu weye ulemavu kupata ruzuku kwa wale wasioweza kufanya kazi
na kuwapatia mitaji kwa wale watakaokuwa na miradi mbali ya kuwapatia kipato.
Chanzo: Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment