Home » » CHADEMA ZANZIBAR WANG'AKA

CHADEMA ZANZIBAR WANG'AKA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Visiwani Zanzibar, kimedai kusikitishwa na taarifa za baadhi ya wabunge wake kurejea katika vikao vya Bunge Maalumu la Katiba Mjini Dodoma kinyume na msimamo wa chama hicho pamoja na Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).

Taarifa iliyotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Bw. Hamad Yussuf, ilisema kitendo hicho kimedhihirika pasipo shaka kuwa wabunge hao ambao ni wajumbe wa Bunge hilo, wamekwenda kinyume na maadili ya chama na kanuni za mwenendo wa maadili ya wabunge wa CHADEMA.

Alisema kwa mujibu wa Katiba ya chama vifungu vya 2.0(a) na 3.0(b), vinazungumzia kushusha hadhi ya chama mbele ya jamii ya Watanzania na wanachama wao nchi nzima.

"Kitendo hiki hakiwezi kuvumilika na kamwe hatuwezi kulea utovu wa nidhamu uliopita mipaka...wasaliti wa aina hii hawatakuwa na nafasi ndani ya chama chetu.

"Tumepokea kwa masikitiko taarifa za baadhi ya wabunge wa CHADEMA ambao wanaounda UKAWA, kurudi ndani katika shughuli za Bunge la Katiba kinyume na maagizo ya vikao vya chama na makubaliano ya umoja huu," alisema.

Aliongeza kuwa, CHADEMA Zanzibar wanaamini wajumbe hao watapatiwa nafasi ya kujieleza na kuwasilisha utetezi wao ambapo vikao vya katiba vitakaa na kuhakikisha nidhamu na maadili ya chama yanalindwa kwa gharama yoyote.

Chanzo:Majira

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa