Mwandishi wetu,
Pemba-Zanzibar Yetu
Jumla ya mikopo 104
yenye thamani ya shilingi milioni 350 imetolewa kwa wanachama wa MUWAPE Saccos
iliyoko mtemeni Wilaya ya Wete ili wajiendeleze kibiashara na kuweza
kupambana na hali ya umaskini wa kipato katika familia zao .
akizungumza na
mwandishi wa habari hizi huko ofisini kwake mtemani wete mwenyekiti wa saccos
hiyo salim khamis salim amesema kuwa mikopo hiyo imelenga kuwaimarisha kiuchumi
wanachama wa saccos hiyo na hivyo kuunga mkono mpango wa Taifa wa kupunguza na
umaskini MKUZA .
amesema kuwa
wanachama wa saccos hiyo wengi wao wameitikia wito wa serikali yao wa kuwataka
kutotegemea ajira kutoka serikalini , na kwamba MUWAPE saccos imekuwa ni
mkombozi wa wanyonge hasa wananchi wenye kipato cha chini na wanaoishi vijijini
.
aidha amesema katika
kuona kwamba mikopo hiyo inawanufaisha wananchama wake , uongozi wa saccos
umeunda kamati ya ufuatiliaji ambapo kamati hiyo imekuwa ikifanya tathmini juu
ya mtaji wa mkopaji kulingana na kiwango cha fedha anachotaka kukopa
kabla hajapatiwa mkopo .
Mwenyekiti huyo
amesema lengo la baadaye la saccos hiyo ni kufungua benki ya jamii ambayo
itakuwa ikitoa mikopo kwa wananchama yenye masharti nafuu ambapo kila
mwanachama atamudu kukopo na kulipa kwa wakati .
akizungumzia suala la
ujereshaji wa mikopo mshika fedha wa saccos hiyo fatma suleiman khatib
amesema wanachama wanatambua umuhimu wa kurejesha mikopo kwa wakati , kutokana
na elimu waliyopatiwa na uongozi .
muwape saccos
ni muungano wa kampuni 19 za wajasiriamali wa Pemba na imeanzishwa
mwaka 2010 ikiwa na wanachama 39 na hadi kufikia septemba 30
mwaka huu ina jumla ya wanachama 250 .
Blogzamikoa
0 comments:
Post a Comment