Home » » KINARA WA TINDIKALI MBARONI ZANZIBAR

KINARA WA TINDIKALI MBARONI ZANZIBAR

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MAKACHERO wa Jeshi la Polisi Zanzibar,wamefanikiwa kumtia mbaroni mmoja wa washukiwa wa matukio ya tindikali visiwani hapa, Alawi Mohammed Silima (25), mkazi wa Fuoni Melinne nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Ofisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar Inspekta Mohammed Mhina, alisema mtuhumiwa anahusishwa na tukio la kummwagia tindikali Sheha wa Shehia ya Tomondo mjini Zanzibar, Mohammed Omar Saidi Kidevu kabla ya kutoweka.

Inspekta Mhina alisema, mtuhumiwa huyo ambaye kwa muda mrefu alikuwa akisakwa na Polisi kwa kuhusiana na tukio hilo, alikamatwa juzi usiku akiwa mafichoni katika eneo la Fuoni baada ya taarifa za kiintelijensia kubaini kuwepo kwake.

Bado Makachero hao wanaendelea kumhoji mtuhumiwa huyo kwa lengo la kubaini mtandao mzima wa matukio mbalimbali ya kiwemo ya tindikali yaliyotokea siku za nyuma visiwani humo.

Kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kunatokana na taarifa za siri za raia wema ambapo Jeshi la Polisi lilikuwa likiendelea na upelelezi wa chini kwa chini ili kumbaini mtuhumiwa na mahali alipojificha.

Tukio la kumwagiwa tindikali kwa Sheha huyo, lilitokea saa 2.45 usiku Mei 22, mwaka jana, wakati alipokuwa akirudi nyumbani akitoka kuchota maji nyumba jirani

Chanzo;Majira

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa