Home » » KUTOKA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR

KUTOKA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mh. Muhamed Aboud (katikati),akizungumza na mwakilishi wa Wawi CUF,Saleh Nassor Juma kushoto huku Mwakilishi wa Kiembesamaki na Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akisikiliza mazungumzo hayo baada ya mapumziko ya kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea hapa Zanzibar huko Chukwani.
MJUMBE wa Baraza la Wawakilishi jimbo Magomeni (CCM) Salmin Awadh Salmin (kushoto),akizungumza na mjumbe wa baraza hilo Ali Mzee Ali (kuteuliwa na Rais) wakati wa kikao cha asubuhi cha baraza huko Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
MWAKILISHI wa Jimbo la Dimani ambae ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Mh. Mwinyihaji Makame,kulia akizungumza na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi,Makaazi ,Maji na Nishati Ali Halil Mirza kwenye vikao vya Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Zahra Ali Hamad,wakibadilishana mawazo na Mwakilishi wa Kwamtipura Hamza Hassan Juma nje ya ukumbi wa Baraza la Wawakilishi leo. (Picha na Abdallah Masangu).

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa