Home » » Mnyaa wa CUF apoteza jimbo.

Mnyaa wa CUF apoteza jimbo.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Jimbo lake lafutwa na tume, baadhi ya waliogombea majimbo ya zamani sasa yamebadilishwa majina.
Muhammed Habibu Mnyaa.
Chama cha Wananchi (CUF) kimetangaza wagombea wa nafasi ya ubunge na uwakilishi kwa majimbo 54 ya uchaguzi kwa nafasi na uwakilishi na majimbo 50 kwa nafasi ya ubunge huku kikimtema kigogo wake, Muhammed Habibu Mnyaa (pichani), baada ya jimbo lake la Mkanyageni kufutwa na Tume ya Uchaguzi (Zec).
 
Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama hicho, Omar Ali Shehe, alisema baada ya Zec kufanya mabadiliko ya mgawanyo wa majimbo na kuongeza majimbo manne mapya, chama hicho kililazimika kufanya mabadiliko ya wagombea wa majimbo.
 
Alisema baadhi ya wagombea waliogombea majimbo ya zamani na sasa yamebadilishwa majina wamewapa majimbo hayo yaliobadilishwa majina na kuwaongeza wagombea wanne kwa majimbo mapya kwa nafasi za uwakilishi.
 
Mnyaa alikataliwa na wananchi katika kura za maoni, lakini baadaye Baraza Kuu la Uongozi likapitisha jina lake kugombea nafasi hiyo, hatua iliyoibua malalamiko kutoka kwa wanachama wa CUF kwa madai ya kuwa hakuwa chaguo lao.
 
Baraza Kuu la CUF lilirejesha jina la Mnyaa kabla ya Zec kutoa ripoti ya mapitio na mgawanyo wa majimbo na baada ya kumaliza kazi hiyo tume ililifuta jimbo la Mkanyageni alilokuwa akiliongoza.
 
Shehe alisema jana kuwa utaratibu uliotumika katika kuwapata wagombea wa majimbo mapya wamefuata katiba ya chama ambayo inaruhusu kufanya mabadiliko katika hali ya dharura.
 
Aidha, CUF imemrejesha Naibu Naziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati, Haji Makame Mwadini ambaye alibwagwa katika kura za maoni kutetea nafasi yake  ya uwakilishi kwa jimbo la Nungwi na jina lake halikurejeshwa na Baraza Kuu la chama hicho, lakini sasa amepewa kugombea jimbo la Kijini.
 
Waliobadilishwa majimbo baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kutaja majina mapya kwa baadhi ya majimbo ni Mji Mkongwe, Ismail Jussa Ladhu (sasa Malindi) wakati ni Ali Saleh aliyekuwa anagombea ubunge Mji Mkongwe (sasa Malindi).
 
Wengine ni mwakilishi wa jimbo la Mtoni, Nassor Ahmed Mazrui amepelekwa  jimbo la Mtopepo, Mansour Yussuf Himid uwakilishi jimbo la Chukwani badala ya Kiembe Samaki na Abdillahi Jihadi Hassan uwakilishi jimbo la Mwanakwerekwe badala ya Magogoni
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa