Mkurugenzi wa Idara ya Elimu akiongea na wanafunzi mapema leo
Wanafunzi wakiwa wanasikiliza kwa umakini Mkurugenzi wa Elimu ya juu zanzibar Leo
*****
Mkurugenzi wa Elimu ya Juu Zanzibar ambae aliambatana na Meneja wake leo wamefika chuo Kikuu cha Zanzibar wakizungumzia matatizo mbali mbali ambayo yanakumba wanafunzi hao chuoni hapo.
Pamoja na mazungumzo yaliyo dumu kwa masaa mawili mkurugenzi huyo alieleza kwa kina matatizo ya bodi ya elimu ya wanafunzi Zanzibar na mambo mbali mbali.
Hata hivyo wanafunzi walipata nafasi ya kuuliza maswali Mbali mbali lakini hayakuweza kujibiwa kama walivyo tarajia kwa kuwa walikuwa na hamu ya kuhoji maswala mengi.
Habari na mwakilishi wetu kutoka Zanzibar
Yassir Matsawily
0 comments:
Post a Comment