Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Uchaguzi wa marudio wa Zanzibar ambao umepangwa
kufanyika Machi 20, mwaka huu, umesababisha Chama cha wananchi (CUF)
kushindwa kufanya maadhimisho ya kuwakumbuka wenzao waliofariki dunia
mwaka 2001.
Maadhimisho hayo hufanyika Januari 27 ya kila mwaka yakishirikisha viongozi wakuu wa chama hicho pamoja na wafuasi wake.
Akizungumza na Nipashe jana, Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi
wa chama hicho Taifa, Abdul Kambaya, alisema uongozi wa CUF taifa
hautafanya maadhimisho hayo kwa kuwa siku hiyo Kamati Ttendaji itakuwa
inafanya kikao cha kujadili tarehe ya marudio ya uchaguzi ambayo
ilitangazwa hivi karibuni na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (Zec).
Kambaya alisema siku hiyo kamati itakutana kuandaa ajenda kuhusiana
na kutangazwa kwa tarehe hiyo ya uchaguzi ambazo zitapelekwa katika
Baraza Kuu la chama.
“Ni vijana tu ndiyo watafanya maadhimisho hayo kwa upande wa
Zanzibar na ndiyo ambao watafanya maandamano ya kukumbuka mauaji hayo.”
Maandamano hayo yamekuwa yakifanyika kila mwaka kama kumbukumbu ya
kuomboleza vifo vya wafuasi wa chama hicho waliouawa Januari 27, mwaka
2001 wakati wa maandamano ya kupinga matokeo ya urais visiwani humo.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment