Home » » KIINI CHA NAULI JUU DAR - ZANZIBAR CHAELEZWA

KIINI CHA NAULI JUU DAR - ZANZIBAR CHAELEZWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Imeandikwa na Khatib Suleiman, Zanzibar


TATIZO la uhaba wa vyombo vya usafiri kati ya Zanzibar na Tanzania Bara ikiwemo boti zinazokwenda kwa kasi, kwa kiasi kikubwa kumechangia kuwepo kwa tatizo la ulanguzi wa tiketi kwa abiria na kusababisha usumbufu mkubwa.
Ulanguzi wa tiketi hizo umeshuhudiwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Ujenzi na Uchukuzi, Mohammed Ahmada wakati alipofanya ziara katika eneo la bandari ya Malindi.
Tiketi moja ya boti zinazokwenda kwa kasi zinazomilikiwa na Kampuni ya Azam Marine inayouzwa Sh 20,000 hupanda bei na kufikia Sh 30,000 hadi 40,000.
Ahmada, akizungumza jana alionesha kukerwa na tatizo hilo na kuahidi kulifanyia kazi kwa sababu linaleta usumbufu mkubwa kwa wananchi, wakiwemo kinamama na wazee.
Alisema ingawa tatizo hilo limechangiwa kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa vyombo vingi vinavyofanya safari kati ya Zanzibar na Tanzania Bara, lakini isiwe sababu ya kupandisha bei kwa kiwango hicho na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi wenye kipato cha chini.
Meneja wa Usafiri wa Kampuni ya Azam Marine, Ali Mohamed Abeid alikiri kuwepo kwa tatizo la tiketi za magendo ambalo wamekuwa wakipambana nalo kwa kiwango kikubwa.

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa