Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Is-haka Omar, Zanzibar.
CHAMA Cha
Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimewasihi viongozi wake kutojali wala
kukatishwa tamaa na maneno yanayotolewa na baadhi ya watu wasiopenda
maendeleo ya Chama hicho badala yake wayatumie kama fursa ya kuongeza
kasi ya utendaji wa majukumu yao.
Nasaha hizo
zimetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Nd. Vuai Ali Vuai
wakati akizungumza na Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Mjini Kichama wakati
kuhitimisha ziara ya kuimarisha uhai wa Chama iliyofanyika katika Mikoa
yote kichama Unguja na Pemba.
Amefafanua kuwa
kuna kauli na njama zisizofaa zinazotolewa na wapinzani wakiwatuhumu
baadhi ya viongozi wa chama kuwa walihusika na njama za kuharibu
Uchaguzi Mkuu uliopita jambo ambalo sio la kweli.
Alisema kauli
hizo zisiwavunje moyo viongozi wa CCM hasa wa Mkoa huo bali wazitumie
kama sehemu muhimu ya kujiongeza kiuongozi na kubuni njia mpya za
kiutendaji zitakazosaidia Wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi
zinazofanywa na Chama hicho.
“ Tuendelee
kufanya kazi kwa bidii na kwa mujibu wa miongozo ya Katiba na Kanuni za
Chama Chetu, wala tusiyape nafasi ya kututawala maneno na kauli za
wapinzani kwani wanakesha wakipanga njama za kila aina ili tupoteze
muelekeo wa kisiasa lakini kwa uwezo wa Mungu hawatoweza kamwe.”,
alifafanua Vuai.
Aidha alisema
Chama hicho kina uzoefu mkubwa wa kisiasa na kinajivunia maendeleo
yaliyopatikana kutokana na viongozi wake walio Mikoani na Wilayani ambao
kwa nyakati tofauti wamekuwa wakiwasimamia kwa uadilifu na weledi
viongozi waliopo chini yao.
Nd. Vuai
aliwambia viongozi kuwa pamoja na kuwepo na changamoto mbali mbali
katika Mikoa yao bado wana jukumu la kufanya kazi kwa bidii kwa lengo
kuimarisha Chama ndani ya maeneo yao.
Aliwataka
viongozi na watendaji wa Chama Cha Mapinduzi Kuongeza kasi ya kutafuta
wanachama wapya ambao wametimiza umri kisheria ili waweze kujiunga na
CCM kwa lengo la kukipigia kura Chama katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Hata hivyo
alisisitiza suala la kuhamasishwa kwa viongozi watakaopewa majukumu ya
kusimamia Uchaguzi wa Chama wasiwanyime fursa wanachama wenye nia na
sifa za uongozi kugombea nafasi mbali mbali ndani ya CCM.
Naibu Katibu
Mkuu huyo, aliwapongeza viongozi wa Mkoa huo kwa kufanikisha Uchaguzi
Mkuu uliopita na kupatikana viongozi makini wa CCM pamoja na kusimamia
ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2015/2020 kwa wananchi wote bila ya
ubaguzi.
Pamoja na hayo
aliwataka Wana CCM na Viongozi wote wa Chama hicho kuendelea na
Maandalizi ya kuandaa mazingira mazuri ya kukipatia ushindi katika
Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020.
Ziara hiyo
imefanyika katika Mikoa yote kichama ya Zanzibar, kwa lengo kuimarisha
chama, kuzungumza na kubadilishana mawazo na viongozi pamoja kuwashukru
na kuwapa pole Wana CCM waliofanyiwa fujo, hila na kujeli na wapinzani
kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu uliopita.
0 comments:
Post a Comment