MAKAMU
Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi (BLM), Mhe. Dkt.
Ali Mohamed Shein, kesho tarehe
29/10/2016 anatarajia kukiongoza Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu
ya CCM Taifa.
Kwa mujibu wa
taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC
Zanzibar - Idara ya Itikadi na Uenezi, Mhe. Waride Bakar Jabu, amesema kikao
hicho cha kawaida cha siku moja kitafanyika Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui
kuanzia saa 4:00 asubuhi.
Amesema kikao
pamoja na mambo mengine, kitapokea na kujadili taarifa mbali mbali kutoka Idara
na Vitengo vya Chama hicho na kuongeza kuwa maandalizi yote yamekamilika.
Aidha, Katibu
Waride amesema kikao hicho kilitanguliwa na Kikao cha Sekretarieti ya Kamati
Maalum ya NEC, kilichokutana tarehe 26 Octoba, mwaka huu, chini ya Mwenyekiti
wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Mhe. Vuai Ali Vuai, kwa lengo la kuandaa
Agenda za kikao hicho.
“KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI”
……………..
Waride Bakar
Jabu
Katibu wa Kamati
Maalum ya NEC
Idara ya Itikadi
na Uenezi - CCM
ZANZIBAR.
28/10/2016
0 comments:
Post a Comment