Home » » Chanjo ya watoto yamsikitisha DC wa Wete

Chanjo ya watoto yamsikitisha DC wa Wete

Mkuu wa Wilaya ya Wete Omar Khamis Othman amesikitishwa na taarifa za matokeo ya chanjo ya watoto katika Wilaya hiyo na kuutaka uongozi wa Wizara ya Afya Wilayani humo kuandaa mipango itakayofanikisha kupata mafanikio katika zoezi la chanzo mwaka huu .
 
Akizundua wiki  ya chanjo ambayo huadhimishwa na nchi za Afrika kuanzia april 22 hadi april 27 , amesema kuwa kiwango cha matokeo ya chanjo kwa mwaka jana si mazuri na kwamba Wizara inatakiwa kuongeza uhamasishaji kwa wananchi ili kuwapeleka watoto kupata chanjo .
 
Amesema katika mwaka jana Wilaya ya Wete ilifanikiwa kutoa chanjo wa watoto asilimia 85 ikiwa ni pungufu ya asilimia kumi yaa maelngo yaliyowekwa na shirika la kuhudumia watoto la ulimwenguni UNECEF
 
Aidha amewataka watendaji wa Wizara Afya  Wilayani humo kuwa mfano wa kuigwa kwa kuwa msitari wa mbele kuwapeleka watoto zao pamoja na kuwahimiza ndugu zao wa karibu kwenda kupatiwa chanjo hiyo .
 
Kwa upande wake Afisa wa Afya Wilaya ya Wete Dk Ali Rashid amesema kuwa pamoja na kuadhimisha Wiku ya chanjo Afrika lakini huduma hizo zinaendelea kitolewa katika Hospitali na vituo vya afya katika Wilaya hiyo.
 
Amesema kuwa katika Wilaya ya Wete kuna vituo 19 vinavyotoa huduma ya chanjo na  wanaimani ya kupata mafanikio katika zoezi la chanjo kutokana na jamii kuhamasika kutokana na elimu inayotolewa na watendaji wa Wizara paamoja na viongozi wa kamati za afya za shehia .
 
Maadhimisho ya wiki ya chanjo Barani Afrika yalianza kuadhimishwa mwaka 1980 ambapo Serikali ya Mapinduzi iliridhia maadhimisho baada ya kuona kuwa watoto wengi wanapotesha maisha .

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa