Mkuu wa Mkoa wa
Kaskazini Pemba Mh Dadi Faki Dadi amewataka Wakuu wa Wilaya ya Wete na
Micheweni kuwaarifu Masheha kuchukua hatua za kisheria dhidi ya
watu wanaojihusisha na vitendo vya ununuzi na uuzaji wa karafuu mbichi na kavu
na kwamba atakayebainika atachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria .
Amesema kuwa Serikali
ya Mkoa haitamuonea huruma Sheha yeyote ambaye vitendo vya ununuzi na uuzaji wa
karafuu vitabainika kuendeshwa katika eneo lake , na kuwataka kuwa makini
katika kulinda uchumi wa Nchi .
Aidha Mh Dadi ,
amesema kuwa watu wanaojihusha na biashara ya magendo ya karafuu wanapaswa
kudhibitiwa na kila mwananchi lakini masheha wao wanatakiwa kuzungumza na
wananchi wao na kuwapa tahadhari hiyo mapema kabla ya sheria kuchukua mkondo
wake .
Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa katika kufanikisha udhibiti wa magendo ya karafuu , vyombo vya ulinzi vimejipanga kikamilifu ili kuona hakuna mwanya unaotumika kusafirisha karafuu kwenda nje ya nchi ambapo tayari jeshi la Polisi limeagizwa kuweka vizuizi vya barabarani (Road Block) ili kudhibiti wanaosafirisha karafuu kutoka eneo moja kwenda eneo jengine bila ya kufuata taratibu .
Amefahamisha kwamba
mwananchi anayetaka kusarifisha karafuu kutoka Shehia moja kwenda nyingine
anatakiwa kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya hivyo .
Shehia ya Mtambwe
Kaskazini katika Wilaya ya Wete bado vitendo vya uuzaji na ununuzi wa karafuu
mbichi na kavu kwa njia ya vikombe pamoja na wizi wa karafuu katika mashamba ya
wakulima vimekithiri .
0 comments:
Post a Comment