Home » » WAANDISHI WA HABARI WAPEWA SOMO JUU YA USAJILI WA ARDHI

WAANDISHI WA HABARI WAPEWA SOMO JUU YA USAJILI WA ARDHI


 Mtalamu wa mambo ya Habari kutoka Smole Bw. Ali Rashid Salim akifahamisha kitu katika mafunzo ya wandishi wa Habari juu usajili wa Ardhi,katika ukumbi wa Wizara ya Habari kikwajuni Mjini Unguja jana.
 Afisa mtambuzi wa Ardhi Unguja Shawana Soud Khamis akitoa elimu ya Utambuzi, kuisajili na kuitumia Ardhi kwa wandishi Habari katika ukumbi wa Wizara ya Habari kikwajuni Mjini Unguja jana.

Baadhi ya wandishi Habari wa vyombo mbalimbali wakisikiliza kwa makini mafunzo yanayotolewa na Mtalamu wa mambo ya Habari kutoka Smole Bw. Ali Rashid Salim (hayupo pichani) katika ukumbi wa Wizara ya Habari kikwajuni Mjini Unguja jana. (Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).
========  =======  =======
Maryam Fumu na Patima Mtumwa Maelezo- Zanzibar.

Afisa Mkaguzi wa Ardhi Zanzibar Shawana Suod Khamis amewataka wananchi kutoa mashirikiano  katika kufanikisha zoezi zima  la  Utambuzi na usajili wa ardhi nchini.

Kauli hiyo imetolewa jana  katika ukumbi wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo wakati akifunga mafunzo ya siku moja ya utambuzi  na usajili wa ardhi kwa  waandishi wa habari .

Alisema  kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuweza kuwapa mbinu za kisasa  na  uwelewa mpana  kwa  waandishi ili kuweza kuihamasisha jamii kuhusiana na zoezi  hilo.

Alieleza kuwa  Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kushirikiana  na Serikali ya Finland  kupitia mradi wa SMOLE II unaendelea na zoezi la usajili wa Ardhi kupitia maeneo mbali mbali ya Zanzibar.

 Shawana ameyataja   baadhi ya maeneo  ambayo tayari yameanza zoezi hilo  na kuonyesha mafanikio kuwa  ni   Kijiji cha Nugwi , Jendele, Paje,  Chwaka, Kwaalinatu ,Mji Mkongwe, Mkokotoni ,Mwembetanga , Rahaleo, Muembeladu,  Muembeshauri, Gulion,  Kibondeni, Kisima  Majongoo, Mchangani na Vikokotoni .

Akieleza baadhi ya faida za usajili wa ardhi  kuwa  ni kupunguza migogoro inayotokea mara kwa mara katika jamii na kumsaidia mmiliki wa ardhi katika  kupata mikopo katika benki,  mashirika na taasisi mbali mbali.

Mkufunzi wa mafunzo hayo Afisa Habari  na Mawasiliano wa SMOLE  Ali Rashid Salim amesema migogoro mingi ya Ardhi husababisha usheleweshaji wa mirathi kwa jimii hasa  kwa wanawake watoto yatima na watu wenye ulemavu na kupelekea kukosekana kwa haki kwa wahusika.

Zoezi  la usajili wa ardhi limeanza rasmi mwaka 2008 inatarajiwa kuwa  ifikapo mwaka 2015 asilimia 50 ya ardhi yote ya Zanzibar iwe tayari  imeshasajiliwa .

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa