Waziri wa Nchi Ofisi
ya Rais , Tawala za Mikoa na Idara Maalumu za SMZ Mh, Haji Omar Kheir
amewataka watendasji wa halmashauri na mabaraza ya miji kusimamia vyema
matumizi ya fedha za serikali kwa kufuata sheria na taratibu za manunuzi halisi
ya kile kinachonunuliwa .
Amesema kuwa tatizo
ambalo limekuwa likitokea katika Idara ka kuwepo na upotevu wa fedha za
serikali ni kutokana na kutokuwepo na wataalamu wa kada ya uhasibu na manunuzi
katika Idara hizo .
Akizungumza kwa
nyakati tofauti na masheha na madiwani na watendaji wa halmshauri na mabaraza
ya miji wa Mkoa wa Kaskazini Pemba , amesema kuwa kamwe hatokuwa tayari kuona
kuwa fedha za serikali zinatumika kinyume na ilivyokusudiwa na atakuwa tayari
kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria .
Amesema kuwa kila
mmoja anapaswa kuheshimu sheria No 5 /2005 ambayo inaongoza suala la
manunuzi na matumizi kwa Idara za Serikali na kuwataka kushirikiana pamoja
katika utendaji wa kazi lakini sio kwa kufichiana maovu .
Aidha
amewasisitiza watendaji wa baraza na mji na halmashauri kuvitambua vyanzo vyao
vya mapato Ili iwe rahisi kuweza kukusanya mapato na kutimiza azma ya
ukusanyaji wa mapato ya kutosha kwa mujibu wa malengo ya bajeti zao .
Mapema akizungumza
katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mh , Dadi Faki Dadi
amewataka Watendaji wa Serikali katika mkoa huo kila mmoja kwa mujibu wa nafasi
aliyonayo , kuwajibika ili kuhakikisha Mkoa kupitia idara au taasisi unapata
maendeleo .
Akitoa ufafanuzi juu
ya suala la vitambulisho vya mzanzibar mkaazi , amewataka madiwani kutoogopa
kuwaambia ukweli wananchi juu ya utaratibu wa kujiandikisha kwenye daftari la
sheha ili kuondoa lawama za kutotambuliwa na masheha .
Amesisitiza kwamba
suala la vitambulisho ni jambo ambalo kila mwanachi mwenye sifa anahaki ya kupewa
ikiwa atafuata sheria na taratibu zilizowekwa .
0 comments:
Post a Comment