Home » » DKT. SHEIN AMTOLEA UVIVU MAALIM SEIF

DKT. SHEIN AMTOLEA UVIVU MAALIM SEIF

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraz a la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein,amesema kauli zinazotolewa na Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif  Sharif Hama d juu ya mchakato wa Katiba Mpya hasa kwenye suala la Mu ungano ni maoni yake binafsi si msimamo wa Serikali au Wazanzibari.
   Alisema licha ya Katiba kutoa uhuru wa kujieleza, hakuna kiongozi anayeweza kuwa na uwezo wa kuw asemea wananchi wa Zanzibar katika mchakato wa Katiba hasa kuhusu Muundo wa Serikali.
Dkt.Shein aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar jana alipozun gumza na waandishi wa habari ili kuelezea maen deleo ya Serikali katika kipindi cha miaka mitatu .
Aliongeza kuwa , kwa mujibu wa Katiba ya nchi, kiongozi mwenye mamlaka ya kuwasemea Wazanzibar ni yeye pekee si vinginevyo.
Kauli hiyo ya Dkt. Shein ,imekuja siku chache baada ya Maalim Seif kunukuliwa na vyombo vya habari akitoa ms imamo wa Wazanzibari kuhusu Muundo wa Muunga no na suala zima la kupigania mamlaka kamili ya Zanzibar na kutaka Serikali tatu.
“Kila mtu kwenye Katiba ana haki ya kusema lakini Maalim Seif hawezi kuisemea Serikali,anayosema kuhu su Muundo wa Serikali ni maoni yake na chama chake, yeye si Msemaji wa Serikali, mimi ndiyo msemaji,” alisema Dkt .Shein,baada ya kuulizwa msimamo wake kuhusu kauli tata zinazotolewa na Maalim Seif.
Licha ya hali hiyo, Dkt. Shein alisema katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa, hakuna tofauti bali jambo la msingi ni kuvumiliana badala ya kila mtu kufanya anavyotaka.
Akizungumzia mafanikio katika kipindi cha miaka mitatu, alisema maendeleo makubwa yamepatika na katika Nyanja mbalimbali,kuboresha huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya,maji na miundombinu.
Matukio ya tindikali
Akizungumzia matukio ya umwagiaji watu tindikali, Dkt. Shein alisema Serikali imekuwa ikichukua hat ua mbalimbali za kukabiliana na wahalifu hao na kusisiti za kuwa, kamwe hawatarudi nyuma kupambana na wahalifu hao.
Alisema matukio hayo yalianza mwaka 199 5 ambapo kijana mmoja Mjini Wete, alimwagiwa tindikali na kusisitiza kuwa, Serikali itaendelea kuwasaka na kuwafikis ha katika vyombo vya sheria watu wote watakaojih usisha na vitendo hivyo.
Suala la ubaguzi
Dkt. Shein alisema,vitendo vya kibaguzi vinavyodai wa kufanywa na baadhi ya watu visiwani humo kutoa kauli za kuwabagua wananchi wa Pemba, wanaofanya vitendo hivyo wakibainika , watachukuliwa hatua.
Alisema tayari ameviagiza vyombo vya dola kufuatilia nyendo za baadhi ya viongozi wa dini wanaod aiwa kuchochea mgawanyiko kwenye jamii.
SektayaU chumi
Alisema juhudi kubwa zinazochukuliwa na Serikali kuimarisha ukusanyaji wa mapato,uwezeshaji na ush irikishaji wananchi katika harakati za kujenga uchumi.
Aliongeza kuwa,ukusanyaji wa mapato ya ndani umeongezeka ambapo mwaka2010/2011 walikusanya sh. bilioni 181.4, mwaka 2011/2012 sh. bilion I 212 na mwaka 2012/13 ukusanyaji ulikuwa sh. Bilioni 266.2.
“Uchumi wetu unakua kila mwaka, ulikuwa kwa asilimia 6.4 mwaka 2010, mwaka 2011 ulifikia asilimi a 6.7 na 2012 ulikua kwa asilimia 7.0,mwaka huu utafikia asilimia 7.5,” alisema.
Sektaya Miundombinu
Aliongeza kuwa, Serikali yake imeweza kutekeleza vyema Ilani ya CCM ya mwaka 2010/2015, Dira 2020 na MKUZAII katika sekta ya miun dombinu kwa kujenga barabara mpya ambazo waliziahidi na nyingine kuzikarabati.
Sekta ya Elimu
Dkt.Shein alisemani dhahiri kuwa maendeleo katika nchi yoyote yanategemea fursa na elimu bora wanay oipata wananchi wake hivyo Serikali yake imeimarisha sekta ya elimu kwa maendeleo ya nchi,kuongeza idadi  ya shule na walimu.
Sektaya Afya
Alisema ujenzi wa vituo 134 vya afya, vimepunguza tatizo la wananchi kutembea umbali mrefu ili kufuata huduma ambazo hivi sasa zimeimarika.

Chanzo;Majira

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa