Home » » Masheikh wapewa masharti magumu ya dhamana

Masheikh wapewa masharti magumu ya dhamana

Baadhi ya watuhumiwa 10 wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) wakiwa katika moja ya Dua ya kuwaombea watu waliokufa katika ajali ya Mali ya Mv. Skagit iliyotokea mwaka juzi 2012 na kuuwa watu kadhaa.
Baadhi ya watuhumiwa 10 wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) wakiwa katika moja ya Dua ya kuwaombea watu waliokufa katika ajali ya Mali ya Mv. Skagit iliyotokea mwaka juzi 2012 na kuuwa watu kadhaa.


ZANZIBAR: Mahkama Kuu Vuga Mjini Zanzibar imetoa dhamana na masharti magumu kwa viongozi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) ambao walisekwa rumande kwa zaidi ya mwaka sasa.
Akisoma hukumu Jaji wa Mahakama hiyo Fatma Hamid Mahmoud aliwataka kila mshitakiwa kutoa fedha taslim milioni 25 kuwa na wadhamini watatu ambao mmoja wao awe ni mfanyakazi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na awe na mali isiyo hamishika yenye thamani hiyo hiyo ya milioni 25, na barua ya kiongozi wa mtaa (Sheha).
Hata hivyo licha ya dhamana hiyo uwzekano wa washitakiw ahao ambao wanatakiwa kurudi mahamani 25 mwezi ujao utekelezaji wa dhamana hizo umekuwa ni mgumu na wamerudishwa rumande huku jamaa zao wakihanngaika kutimiza masharti hayo. Huyu hapa Wakili wa watuhumiwa hao Abdallah Juma anasema.
Masharti mengine ni kuwa na kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi, kuwasilisha hati ya kusafiria (Passport) Mahakamani na kutoruhusiwa kusafiri hata kuvuka katika kisiwa cha Unguja bila ya ruhusa ya Mahakama pamoja na washitakiwa hao kutoruhusiwa kuzungumza na waumini wao kwa njia ya mihadhara ya nje wala misikitini isipokuwa ruhusa ni kusaidilisha isiwe zaidi ya hapo.
Kutofanya wala kusababisha vitendo vyovyote venye kuashiria fujo kinyume na hilo watarudi rumande hadi kesi itakapokwisha.
Mapema mwendesha mashitaka wa serikali Rashid Abdallah aliwasilisha pingamizi  mbele jaji huyo za kuzuwia amri ya kuwataka kuwasilisha sababu za kuzuwia dhamana za watuhumiwa hao.
Watuhumiwa hao ni  Farid Hadi Ahmed (41) mkaazi wa Mbuyuni,Mselem Ali Mselem (52) mkaazi wa Kwamtipura, Mussa Juma Mussa (47) mkaazi wa Makadara na Azan Khalid (48) mkaazi wa Mfenesini.
Wengine ni Suleiman Juma Suleiman (66), mkaazi wa Makadara, Khamis Ali Suleiman (59) mkaazi wa Mwanakwerekwe, Hassan Bakar Suleiman (39) mkaazi wa Tomondo, Ghalib Ahmada Juma (39) mkaazi wa Mwanakwerekwe , Abdallah Said (48) mkaazi wa Misufini na Majaliwa Fikirini Majaliwa
Mashtaka waliosomewa washitakiwa hao ni kuharibu mali,  Uchochezi,Ushawishi na kuhamasisha fujo na kosa la tatu ni kula njama ya kufanya kosa.
Kosa la nne likimkabili mshitakiwa namba nne Azan Khalid ambae anadaiwa kutoa maneno ya matusi kwa kamishna wa polisi vitendo vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani ambapo Azzan hakuwepo Mahakamani hapo kitendo kilichomfanya jaji Fatma kuhoji ni kweli mtuhumiwa huyo anaumwa au ni unjanja wa kukosa kwenda mahakamani
“Mbona watuhumiwa hawa ni 9 mmoja yupo wapi hivi ni kweli anaumwa hebu jamaa yake njoo hapa uninongoneze” alisema Jaji Fatma ambapo anayemuwakilish Azzan alisogea na kuongea naye.
Vitendo hivyo vinadaiwa   kufanyika kati ya Oktoba 17,18 na 19 katika maeneo tofauti katika manispaa ya Mji wa Zanziba na kuharibu mali za watu na serikali zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 500.
Kesi hiyo iliakhirishwa  hadi Februai 27 mwaka huu na watuhumiwa walirudi rumande hadi watakapokamilisha masharti ya dhamana zao huku jamaa za watuhumiwa hao wakionekana kukimbilia majumbani na kuhangaikia kupatikana kwa fedha hizo.
Akizungumza nje ya Mahakama hiyo Wakili wa upande wa Watuhumiwa Abdallah Juma alisema masharti waliopewa wateja wake ni magumu mno na hivyo hadhani kama wanaweza kuyatekeleza katika kipindi walichopewa.
“Masharti yaliotolewa ni magumu kutekelezeka na kisheria masharti hayatakiwi yawe magumu kiasi kama hicho kwa kuwa dhamana ni haki ya kila mmoja wetu na hivyo kupewa masharti magumu kiasi hicho haipendezi lakini kwa kuwa Mahakama imeshaamua basi tutafata utaratibu na tutarudi tena Mahakamani kuiomba mahakama ipunguze masharti hayo” aliongeza Wakili huyo.
Wakili huyo amesema madhumuni ya kupewa dhamana sio kumkomoa bali ni kumfanya mshitakiwa aweze kufika mahakamani hivyo bado wao kama mawakili wana matumaini ya kurudi tena mahakamani na kuishawishi mahakama iweze kupunguza masharti hayo ambayo ni magumu.
Chanzo;Zanzibar yetu

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa