Home » » Ndoto kubinafsisha karafuu yafutika

Ndoto kubinafsisha karafuu yafutika

Ndoto za karafuu kubinafsishwa Zanzibar imetoweka baada ya Waziri wa Biashara ,Viwanda na Masoko, Nassor Ahmed Mazrui kuwasilisha muswada wa sheria unaoipa nguvu Serikali kudhibiti zao hilo.
Pia, unaweka adhabu kali kwa mtu yeyote atakayepatikana na hatia ya kuhujumu zao la karafuu au miti yake. Mswada huo unafuata Sheria ya Karafuu Namba 11 ya mwaka 1985 na kuweka sheria mpya ya maendeleo ya karafuu, ikiwamo kuanzishwa kwa mfuko wa maendeleo ya zao hilo visiwani Zanzibar na kuweka masharti ya ukaushauji na kupiga marafuku kuanikwa juu ya paa za nyumba.
Waziri Mazrui alisema kutakuwa na kikosi kazi kitakachoteuliwa na kuongozwa na waziri, kifanya kazi zinahusiana na uzalishaji, uuzaji na uendelezaji karafuu na kazi nyingine kitakazopewa na waziri au bodi.
Alisema kifungu cha 13(1) kinakataza kwa mtu yeyote kufanya vitendo vya kuchoma miti ya karafuu, kutengeneza mkaa, kuangusha, kung’oa mkarafuu, kuchimba mchanga au udongo kwenye shamba la mikarafuu au kufanya shughuli nyingine yoyote inayokatazwa na kanuni kwa maendeleo ya zao hilo.
Pia, Waziri Mazrui alisema ni marufuku kutumia mkarafu kwa ujenzi wa aina yoyote iwe mbao. kuchonga vinyago au mapambo na atakayetaka kukata mkarafuu kwa madhumuni ya maendeleo ataomba kibali kwa waziri.
Hata hivyo, Waziri Mazrui alisema mtu yeyote atakayekwenda kinyume na sheria hiyo akipatikana na hatia, atalipa faini si chini ya Sh5 milioni au kifungo cha miaka mitano au adhabu zote kwa pamoja kulingana na uzito wa kosa.
Pia, sheria hiyo imempa uwezo waziri kutangaza katika Gazeti la Serikali ndani ya Zanzibar kuwa, ni eneo la upandaji karafuu na mtu yeyote atakusudia kuhamisha karafuu kavu au mbichi au makonyo ya kutoka sehemu moja kwenda nyingine lazima awe na kibali cha sheha.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa