Kikosi cha Simba kilichoshiriki kombe la Mapinduzi mjini Zanzibar.
Na Juma Mtanda Blog
SIMBA ambayo haijapoteza mchezo wowote tangu kuanza kwa Kombe la
Mapinduzi, ikiichapa KCCA ya Uganda leo Jumatatu kwenye mchezo wa
fainali itachukua mamilioni yaliyotolewa na Yanga. Mechi hiyo itakuwa
‘laivu’ kwenye Azam TV 1.
Yanga ilijitoa kwenye mashindano hayo na kutoa Sh
10 Milioni kama kuomba radhi kwa waandaji halafu ikaishia zake Uturuki
kuweka kambi.
Lakini Simba ikishinda kwenye fainali hiyo
itachukua Dola 10,000 ambazo ni kama Sh 16 Milioni za Tanzania. Waandaji
ni kama wanaongezea kiasi kidogo kwenye fungu la Yanga.
Mechi hiyo itachezwa saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Amaan wenye nyasi bandia.
Beki tegemeo wa Simba, Donald Mosoti alisema lengo lao ni kupata bao la mapema sana ili kujiwekea mazingira ya ushindi.
“Tukitaka tushinde hapa ni lazima tuwafunge mapema
KCCA kutokana na timu waliyonayo, unajua hawa jamaa tulicheza nao
katika mechi za kwanza na hatukufungana. Hawa wanatujua na sisi
tunawajua.
“Tukiwafunga watachanganyikiwa halafu watakuwa na
akili moja ya kurudisha bao huku sisi tukijipanga kuongeza la pili,
naongea na wenzangu kuwafahamisha juu ya jambo hili,” alisema Mosoti
mwenye umri wa miaka 29.
Hii ni mara ya pili kwa Simba na KCCA kupambana
katika michuano hiyo, Januari 3, mwaka huu zilikutana katika mechi ya
Kundi B na kutoka suluhu.
Rekodi ya mechi za Simba katika michuano ipo hivi,
ukiondoa suluhu yake na KCCA, imezifunga AFC Leopards bao 1-0, KMKM
1-0, Chuoni 2-0 na URA mabao 2-0.
Simba haijapoteza mchezo ingawa fowadi yake bado
haitishi kutokana na kutofunga mabao mengi hadi wanaingia fainali
wamefunga mabao sita katika mechi tano walizocheza.
Mchezo huo utawakutanisha wakali ambao ni Amir Kiemba wa Simba na Waswa Herman wa KCCA.
Kocha wa Simba Mcrotia, Zdravko Logarusic ametamba
kuibuka na ushindi katika mchezo huo na amewatahadharisha wapinzani
wake kuwa kama watakuwa makini kumzuia Kiemba basi wachezaji wengine
watafunga na kuchukua kombe.
0 comments:
Post a Comment