Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Bunge la Katiba
Kadhalika, wajumbe wengine wawakilishi wa makundi mbalimbali wametakiwa kuacha kunyoosheana vidole kwa kuwa wanaweza kusababisha kupata katiba isiyokidhi matakwa ya taifa.
Mjumbe huyu wa Bunge Maalum la Katiba alisema hayo katika mahojiano na NIPASHE kufuatia na tabia ya baadhi ya wajumbe kutetea vyama na asasi zao.
Alisema: “Tupo kwenye bunge hili kwa ajili ya kuwakilisha Watanzania siyo kwa kuendeleza itikadi ya chama kinachotetea masilahi yake,” alisema.
Mjumbe huyo alisema washiriki wa wananchi wanatakiwa kuingia katika bunge kama taifa moja la Tanzania ili wapate Katiba bora.
Alisema Watanzania wanatarajia kupata katiba hiyo ambayo itatetea na kusimamia kila kundi katika jamii kuanzia ulinzi wa haki za binadamu, urai, uvuvi na kilimo bila ubaguzi.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment