Home » » Serikali 3 yaibua mazito Z’bar

Serikali 3 yaibua mazito Z’bar

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, wametakiwa kuacha tabia ya kuwataja watu wenye asili ya Pemba pekee kuwa ndio wenye msimamo wa kudai Serikali tatu, bali mfumo huo umependekezwa na watu wenye asili tofauti.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Chipukizi wa CCM, Bw. Muhija Ali Kombo, katika kongamano la wana CCM lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita, Mtoni Wilaya ya Magharibi Unguja.
Alisema imekuwa kawaida kwa baadhi ya wanachama wa chama hicho kuwaandama watu
wenye asili ya Pemba na kudai wao ndio wanaotaka Serikali tatu ambapo baadhi ya watu kutoka Chaani, Makunduchi na Kitope wanashabikia mfumo huo.
“Mimi mwenyewe ni Mpemba lakini sishabikii mfumo wa Serikali mbili sasa unaposimama na kumtaja Mpemba kuwa ndo anayeshabikia
Serikali tatu unafanya kosa,” alisema.
Katika kongamano hilo, Bw. Muhija aliwataja baadhi ya viongozi ambao wana asili ya Unguja
lakini wapo CCM pia ni waumini wakubwa wa Serikali mbili.
Aliwataja viongozi hao kuwa ni Mwakilishi wa Jimbo la Kwamtipura, Bw. Hamza Hassan Juma, Jimbo la Kitope Bw. Mbarouk Makame Mshimba na Jaku Hashim Ayuob ambaye ni mwakilishi wa
Jimbo la Muyuni.
“Nimelazimika kuwataja kwa majina kwa sababu ya uchungu nilionao, kila mmoja wetu
anaposimama anatajwa Mpemba lakini mimi, Mwnyekiti wa CCM Mkoa wa Magharibi Bw. Yussuf Mohammed na Bw. Baraka Shamte ni wapemba lakini mbona hatushabikii mfumo wa Serikali tatu,” alisema.
Katika kongamano hilo, wanachama hao walitoa azimio la kuwataka wabunge na wawakilishi
wa CCM kusimama imara na kutetea mfumo wa Serikali mbili vinginevyo watakaporudi watafute
majimbo mengine ya kugombea 2015.
Kongamano hilo liliandaliwa na CCM likiwa na lengo la kutoa maazimio yao juu ya muundo wa
Muungano likitarajiwa kuendelea katika Mkoa wa Kaskazini Machi 29 mwaka huu.

chanzo;Majira

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa