Home » » UN yawakumbusha wanafunzi Utumwa yawapeleka maeneo ya kihistoria visiwani Zanzibar

UN yawakumbusha wanafunzi Utumwa yawapeleka maeneo ya kihistoria visiwani Zanzibar

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
DSC_0017

Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) kutoka Makao Makuu Dar es Salaam Stella Vuzo akitoa ujumbe wa siku ya Kimataifa ya kumbukumbu ya wahanga wa Utumwa na Biashara ya Utumwa ng’ambo ya Bahari ya Atlantiki kwa wanafunzi wa Skuli ya Sekondari ya Ubungo Modern (hawapo pichani) walipotembelea maeneo yaliyokuwa yakiendesha Biashara ya Utumwa Zanzibar.

Biashara hiyo ya Watumwa ilifanyika kwa miaka 400 na kuhusisha zaidi ya Waafrika milioni 15 na watu wenye asili ya Afrika ambao walikuwa waathirika wa ukatili wa Utumwa na kuendelea kuteseka na madhara yaa biashara ya Utumwa.

Bi. Vuzzo alisema lengo la ziara hiyo ni kutaka Wanafunzi kujifunza madhara ya biashara ya Utumwa jinsi ilivyofanyika na madhara yake na ili waweze kusaidia katika jitihada za kuitokomeza biashara hiyo ambayo mpaka sasa bado inaendelea kufanyika kimya kimya katika maeneo mbalimbali nchini na kuwataka kuzijua haki zao za kibinadamu na kutogeuzwa bidhaa za kuuzwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa udanganyifu wa kupelekwa kufanya kazi nchini za kigeni.

DSC_0048

Mtembezaji wageni Peter Mashauri wa Kanisa la Mkunazini akiwapa maelezo wanafunzi wa Skuli ya Sekondari ya Ubungo Modern ya Dar es salaam walipotembelea maeneo ya Kihistoria yaliyokuwa yakiendesha Biashara ya Utumwa Zanzibar katika siku ya Kimatafa ya kumbukumbu hiyo inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo Machi, 25 

DSC_0057

Wanafunzi wa Sekondari ya Ubungo wakimsikiliza mtembezaji wageni (hayupo pichani) wakiwa katika chumba kidogo kilichokuwa kikihifadhiwa watumwa waliokuwa wakisubiri kusafirishwa kwa ajili ya kupigwa mnada katika Kanisa Kuu la Mkunazini.

DSC_0160

Wanafunzi wa Ubungo Modern wakiangalia vitabu vya Historia ya Zanzibar walipotembelea Kasri ya  Wananchi  Forodhani Mjini Zanzibar. 

DSC_0894

Wanafunzi wa Ubungo wakiangalia sehemu waliyokuwa wakihifadhiwa watumwa katika maeneo ya Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.

DSC_0901

Wanafunzi wakiangalia Bandari ndogo iliyokuwa ikitumika kupokelea na  kusafirisha watumwa katika maeneo ya  Mangapwani Mkoa Kaskazini Unguja.
(PICHA NA MAKAME MSHENGA WA MAELEZO ZANZIBAR.)

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa