Home » » MH:DADI FAKI DADI AITAKA WIZARA YA ELIMU PEMBA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WANAFUNZI WATORO MASHULENI

MH:DADI FAKI DADI AITAKA WIZARA YA ELIMU PEMBA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WANAFUNZI WATORO MASHULENI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Zaidi ya wanafunzi 200 kati ya 363 wa shule ya Sekondari ya Msuka Wilaya ya Micheweni  Pemba hawahudhurii masomo  siku ya Ijumaa ya kila Wiki bila ya sababu za msingi .

Waalimu wa shule  hiyo wameyabainisha hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe Dadi Faki Dadi alipofanya ziara aya kuteembelea katika Shule hiyo .

Wamesema kuwa wanafunzi hao wamekuwa na kawaida ya kujipa mapumziko siku ya Ijumaa hali ambayo inachangia matokeo mabaya ya mitihani yao ya Taifa  ambapo wameiomba Serikali ya Mkoa kusaidia kupatikana kwa ufumbuzi wa kitendo hicho .

Akizungumza  na walimu , wanafunzi pamoja na wajumbe wa kamati ya shule hiyo , Mkuu wa Mkoa ameiagiza Wizara ya Elimu Wilaya ya Micheweni kuchukua hatua za kinidhamu dhihdi ya wanafunzi  ambao wameifanya siku ya Ijumaa kuwa ni mapumziko yao .

Amesema kuwa Serikali haiwezi kuona sheria , kanuni na taratibu zinavunjwa hivyo ni lazima suala hilo likomeshwe mara moja ili kuejnga maadili mema kwa wanafunzi .

Afisa Elimu na Mafunzio ya Amali Wilaya ya Micheweni Mbwana Shaame Said amesema kuwa wamepanga kukutana na wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo ili kutafuta njia ya kukabiliana na tatizo hilo .

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa