Home » » MRADI WA ACRA KUNUFAISHA WAZANZIBZRI 15,000

MRADI WA ACRA KUNUFAISHA WAZANZIBZRI 15,000

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
ZAIDI ya watu 15,000 watafaidika na mradi wa pamoja baina ya Jumuiya ya Hifadhi ya Mji Mkongwe na Jumuiya ya ACRA utakaoanza hivi karibuni ili kuendeleza Mji Mkongwe.
 Hayo yalibainishwa na Mohammed Balow, Mwenyekiti wa Jumuiya ya uhifadhi Mji Mkongwe (Zanzibar Stone Town Heritage Society) katika hafla ya kutiliana saini kati yake na Nicola Moganti ambaye ni Mratibu wa Shirika la Maendeleo la ACRA.
 Miongoni mwa  watakaofaidika ni Wazanzibari, mafundi ujenzi 400, watu 75 wasio na ujuzi, wajasiriamali wa sekta ya ujenzi na ambao wamesajiliwa na jumuiya hiyo.
 Mradi huo utaanzisha maabara katika Chuo Kikuu cha SUZA ambapo utasaidia kufanya utafiti unaohusu malighafi zinazotumika kujenga majengo ya kihistoria. 
Mradi huo pia utasaidia kuandikwa kwa mtaala unaohusu kufanya matengenezo ya majengo ya kale ambao mtaala huo utatumiwa na Chuo cha Karume (Karume Institute of Science and Technology) na kufanya mikutano na wadau mbalimbali kuzungumzia masuala ya urithi na utamaduni yakiwemo majengo ya kiasili yaliyopo Zanzibar.
 Jumuiya ya uhifadhi Mji Kongwe ndio itakayokuwa muhusika mkuu katika kupanga na kutekeleza shughuli zinazohusu kutoa taaluma na kukuza uelewa wa masuala ya kihistoria na urithi wa utamaduni uliopo visiwani humo huku ikiandaa na kufanya kampeni kwa skuli zenye lengo la kutoa taaluma kwa ajili ya kukuza uelewa juu ya masuala ya urithi na utamaduni wa Zanzibar. 
Mradi huo wa miaka mitatu wenye lengo la kuhifadhi na kutunza urithi wa utamaduni Zanzibar na kuhifadhi sekta hii kwa kuchangia ukuaji wa uchumi nchini utagharimu jumla ya EURO 1,200,000.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa