Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Wabunge wa Bunge Maalumu la Katiba
Akizungumza na waandishi wa habari,mmoja wa viongozi kutoka Zanzibar, Msim Seifu Abdallah, alisema bunge hilo linayumbishwa na baadhi ya wajumbe wake ambao hawana uzalendo na utaifa na badala yake niwapigania maslahi binafsi.
Msim ambaye ni Diwani wa ya Mfenisini Wilaya ya Magharibi Zanzibar, alisema kuwa baadhi ya wanasiasa ndani ya bunge hilo ni wapiga propaganda na kuwalisha maneno Wazanzibari kuwa wanataka serikali tatu.
Alidai kuwa msimamo wa Wazanzibari ni serikali mbili na siyo tatu kama wanavyosimamia baadhi ya wajumbe wa bunge hilo.
“Wazanzibar bado tunawaenze waasisi wa iliyokuwa Tanganyika, Hayati Mwalimu Nyerere na Zanzibar, Hayati Karume, wao walisimamia serikali mbili……sisi hatuwezi kuwa tofauti na wao, vinginevyo ni propaganda za wanasiasa kutuopakazia maneno ya serikali tatu,” alisema Msim.
Hata hivyo, Msim aliwataka wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kufikilia Tanzania kwanza na kwamba wasitumie nafasi hiyo kwa malumbano kutumika wala maslahi yao binafsi,kikundi au mtu.
Katika hatua nyingine, Msim aliwataka Watanzania bara na Wazanzibar kutosikia maneno yanayokienezwa kuhusu msimamo wa Wazanzibari kuwa ni serikali tatu kwani ni ya uongo na propaganda za wanasiasa
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment