Home » » YAKHE WAKIMBIA NINI ?MJUMBE BUNGE LA KATIBA ADAI WAKITOSA BARA WATAKOSA MAKAZI

YAKHE WAKIMBIA NINI ?MJUMBE BUNGE LA KATIBA ADAI WAKITOSA BARA WATAKOSA MAKAZI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Bila umoja na Tanzania Bara, Wazanzibari wataishia kuwa “wakimbizi” kwani dalili zaonyesha visiwa vyao vitamezwa na Bahari ya Hindi.
Hiyo ndiyo hoja mpya kuhusu mustakabali wa Muungano, iliyoibuliwa leo katika Bunge Maalum la Katiba linaloendelea mjini hapa.
Dokezo hilo limetolewa na aliyekuwa Waziri wa Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Terezya Huvisa katika kikao cha baraza hilo Alhamisi asubuhi.
Mjumbe huyo anadai kuwa viashiria vyaonyesha Unguja na Pemba zaweza kutoweka siku za usoni, hali itakayopelekea wakazi wake kuwa Wakimbizi wa Mabadiliko ya Hali ya Hewa.
“Bila Muungano Zanzibar itakuwa na wakimbizi wa [sic] Climate Change,” amesisitiza Dk. Huvisa.
Suala jingine lilogusiwa Bungeni hapa leo ni umiliki ardhi, huku mjumbe mmoja akidai kuwa kama haki ardhi isipolindwa, atapiga kampeni vijijini ili Rasimu ya Pili ya Katiba isipite.
“Kule kijijini tunapotoka sisi…ukifika tu ukauliza suala la Katiba, utakachoambiwa ni migogoro ya ardhi, maeneo ya malisho [na] miundombinu,” amesema Mabagda Mwataghu anayewakilisha Vyama vya Wafugaji.
Bunge hilo pia lilikumbwa na sintofahamu ya muda mfupi mara baada ya mwakilishi wa Taasisi za Elimu toka Zanzibar, Zeyana M. Haji, kuangua kilio baada ya kupata taarifa za ghafla kuwa baba yake amefariki.
Hali hiyo ilimlazimu Mwenyekiti wa baraza hilo, Samuel Sitta, asitishe mdahalo kwa muda ili kutoa nafasi kwa mjumbe huyo kusindikizwa nje ya ukumbi wa Bunge Maalum.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa