Home » » MAFIA YAWATANGAZIA VITA WANAOWAPA MIMBA WANAFUNZI

MAFIA YAWATANGAZIA VITA WANAOWAPA MIMBA WANAFUNZI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Sauda Mtondoo.PICHA|MAKTABA  
Wilaya ya Mafia imetangaza mkakati wa kuwasaka kwa siri watu wanaohusika na kuwapa mimba wanafunzi ili kuwachukulia hatua za kisheria.
Akizungumza katika mahojiano na mwandishi wa habari hizi, Mkuu wa Wilaya hiyo, Sauda Mtondoo alisema kuwa hatua hiyo inalenga kutetea haki ya watoto wa kike wanaokatishwa masomo kutokana na ujauzito.
“Tatizo la kukatiza masomo kwa mimba lipo hapa Mafia, lakini nimeanzisha mikakati wa kuhakikisha linatokomezwa. Kwa kushirikiana na Shirika la Action Aid, Polisi na walimu tunaendesha mkakati huo wa siri,” alisema Mtondoo.
Alifafanua kuwa hatua hiyo inatokana na wazazi na walezi wengi wa watoto wa kike wilayani humo kushindwa kutoa ushahidi wa matukio ya watoto wa kike kupewa ujauzito sababu kubwa ikiwa uhusiano wa kidugu baina ya aliyepewa ujauzito na mvulana.
“Utakuta aliyempa binti ujauzito ni binamu yake, hapo wazazi huamua kukaa kimya kwani wakitoa ushahidi wanaogopa hatua za kisheria zitaathiri familia,”alisema.
Alibainisha kuwa takwimu zinaonyesha kuwa kesi zisizopungua nne za watoto wa kike kupewa ujauzito hufikishwa mahakamani kila mwaka, lakini ushahidi hukwama.
“Sasa walimu wamekubali watawasiliana kwa siri nami moja kwa moja ili hatua zifuate mkondo kwa siri na katika hilo sina msalie Mtume,” alisema Mtondoo
 Chanzo:Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa