Watoto hawa ni miongoni mwa watoto wengi wanaofanya kazi za kugonga
kokoto na kuchonga matofali kisiwani Pemba. Watoto wengi wanatumikishwa
katika ajira hiyo ngumu, huku wakikosa haki yao ya kupata elimu. Picha
na Talib Ussi.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa Mwananchi kupitia mradi wa
kupambana na ajira ngumu kwa watoto, zaidi ya watoto 15,000
wanajishughulisha na ajira tena zile ngumu.
Wakati Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikitimiza
miaka 50 tangu Mapinduzi ya mwaka 1964 yaliyojenga mazingira mazuri ya
maendeleo, visiwa vya Unguja na Pemba vimeathirika na ajira ngumu
zinazowahusisha watoto.
Hicho ni kikwazo kinachoweza kuifanya Zanzibar
ishindwe kuyafikia Malengo ya Milenia, ambayo yanataka hadi kufikia
mwaka 2015 watoto wote wapate fursa na haki za msingi za elimu.
Vichocheo vya ajira kwa watoto
Kwa Zanzibar sababu ni nyingi, ikiwamo wazazi
kutokuwa na mwamko wa kuwasomesha watoto wao na kutamalaki kwa umaskini
katika familia nyingi.
Hata hivyo, wapo wazazi walioamua tu
kuwatumikisha watoto wao katika ajira ngumu, huku wakisingizia kuwa
wanafanya hivyo kwa sababu ya ugumu wa maisha.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa Mwananchi kupitia mradi
wa kupambana na ajira ngumu kwa watoto, zaidi ya watoto 15,000
wanajishughulisha na ajira tena zile ngumu.
Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake
(Tamwa) ambacho ni sehemu ya washiriki wa mradi, Sheha Haji Dau,
anasema waliwatembelea watoto zaidi ya 264 na kubaini 80 wanaishi katika
mazingira hatarishi kwa kujishughulisha na ajira ngumu.
Baada ya kuwabaini anasema wamekuwa wakihakikisha
wanarudi shule kama anavyosema: “Kijiji cha Charawe pekee watoto 16
wamerudishwa shule. Wanaendelea vizuri na masomo, huku tukitoa elimu kwa
wazazi wafuatilie maendeleo yao. ‘’
Hali mbaya Pemba
Kisiwa cha Pemba kinatajwa kuathirika zaidi kwa
kuwa na idadi kubwa ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi hata
ndani ya familia zao.
Mratibu wa asasi ya kiraia inayoshughulikia
mapambano ya ajira ngumu za watoto katika Mkoa wa Kaskazini Pemba
(Kukhawa), Mgeni Hamad Othman anasema ajira za watoto zimerudisha nyuma
maendeleo ya sekta ya elimu katika kisiwa cha Pemba.
Chanzo;mwananchi
Chanzo;mwananchi
0 comments:
Post a Comment