Home » » MAALIM SEIF ASIFU MCHANGO WA SULTAN QABOOS WA OMAN

MAALIM SEIF ASIFU MCHANGO WA SULTAN QABOOS WA OMAN

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad Aidha   amesifu juhudi zinazochukuliwa na Sultan Qaboos wa Oman katika kuisadia Zanzibar katika Nyanja mbali mbali za kiuchumi na kitaaluma.

Amesema ni jambo la kutia moyo kuona uhusiano na ushirikiano kati ya Oman na Zanzibar unaendelea kuimarika siku hadi siku.

Amesema mbali na uhusiano ya kiserikali, nchi hizo pia zina uhusiano wa kindugu ambao hauwezi kusahauliwa, hali inayopelekea watu wengi wa Oman kuamua kuja Zanzibar kwa ajili ya mapumziko wakati wa likizo zao.

Akizungumza na Balozi mdogo wa Oman Sheikh Saleh Al-Hafidh, aliyefika Ofisini kwake Migombani kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa utumishi, Maalim Seif amesema uhusiano huyo utazidi kuimarishwa kwa maslahi ya pande zote mbili.

Amesifu kazi nzuri iliyofanywa na balozi huyo katika kipindi kifupi cha miezi mitatu alichofanya kazi Zanzibar, ikiwa ni pamoja na kuratibu na kufanikisha kufanyika kwa Tamasha la Kiislamu hapa nchini.

Amemtaka Sheikh Saleh aendelee kuwa balozi wa kuitangaza Zanzibar nchini Oman na nchi nyengine atakazokwenda kuzifanyia kazi.

 Kwa upande wake Balozi mdogo wa Oman Sheikh Saleh Al-Hafidh, ameishukuru Serikali na wananchi wa Zanzibar kwa kumpa mashirikiano mazuri yaliyorahisisha kutekeleza majukumu yake ya kikazi kwa ufanisi.

Amesema ataendelea kushirkiana na Zanzibar wakati wowote licha ya kumaliza muda wake wa utumishi hapa nchini


0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa