Home » » MAALIM SEIF:ASIFIA MAENDELEO SHULE YA ALHAMIS CAMP PEMBA

MAALIM SEIF:ASIFIA MAENDELEO SHULE YA ALHAMIS CAMP PEMBA

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amesifu maendeleo yaliyopatikana katika shule ya msingi ya ALI KHAMIS CAMP inayosimamiwa na Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ).
Amesema shule hiyo imekuwa na maendeleo ya kupigiwa mfano kwa shule za Tanzania, na kwamba yamepatikana kutokana na umakini na nia njema ya jeshi hilo katika kuwapatia watoto elimu bora.
Maalim Seif ametoa pongezi hizo katika shule hiyo, wakati wa ziara yake ya kutembelea taasisi za elimu kisiwani Pemba.
Aidha amesema mafanikio hayo yamepatikana kutokana na mashirikiano makubwa yaliyopo kati ya wananchi, Wizara ya elimu pamoja na Jeshi hilo, sambamba na nia njema iliyopo katika kuwapatia wananchi maendeleo.
Amesema Jeshi la Wananchi ni taasisi muhimu katika kuchangia maendeleo ya nchi, na kwamba vikosi vya (14 na 151 KJ) vimeonyesha mwitikio mzuri wa kushirikiana na wananchi katika jitihada za kujikwamua kimaendeleo.
Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na Jeshi hilo katika kuhakikisha kuwa linatimiza malengo yake ya kuwapatia elimu pamoja na huduma za afya wananchi wa eneo hilo.
Katika ziara hiyo Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad ameahidi kuchangia mifuko 50 ya saraji ndani ya kipindi cha wiki moja, ili kuchangia ujenzi wa shule hiyo, sambamba na kugharamia mafuta yatakayotumika kwa ajili ya usafishaji wa kiwanja cha michezo kwa watoto katika eneo hilo.
Mapema Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Eugene Anathory Ruta amesema mafanikio ya shule hiyo yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na ziara ya Makamu wa Kwanza wa Rais aliyoifanya katika skuli hiyo mwezi Juni, mwaka huu.
Amesema tangu kufanyika kwa ziara ya mwezi Juni, wafadhili kadhaa wamejitokeza kuchangia maendeleo ya shule hiyo, na kwamba sasa wana mpango wa kujenga shule za maandalizi na Sekondari ambazo tayari ujenzi wake umeanza hatua za msingi.
Kwa upande wake kamanda wa kikosi cha (14 KJ) J.K. Mbwelo amesema maendeleo ya shule hiyo hailengi kwa wanajeshi pekee bali kwa jamii nzima iliyowazunguka.
Kwa sasa wananchi wengi wa maeneo ya Machomanne, Wawi na Vitongoji wamekuwa wakipatiwa huduma za matibabu na elimu katika kituo cha afya ya shule katika kambi hiyo ya Ali Khamis Camp.
Maalim Seif pia alitembelea shule ya Sekondari ya Madungu na kuelezea kuridhishwa na maendeleo ya skuli hiyo.
Wakati huo huo akiwa katika shule ya Fidel Castro, Makamu wa Kwanza wa Rais amepongeza hatua ya kutengezwa na kujengwa upya kwa shule hiyo, hatua ambao imeirejeshe hadhi yake ya asili.
Ameuagiza uongozi wa shule hiyo kufanya kazi ya ziada, ili kuhakikisha kuwa ubora wa majengo unakwenda sambamba na matokeo mazuri ya wanafunzi katika mitihani ya Taifa.
Nae Msaidi Mwalimu Mkuu wa shule ya Fidel Castro. Khamis Rashid Nassor, amemuhakikishia Makamu wa Kwanza wa Rais kuwa tayari wameweka mikakati imara kuona kuwa shule hiyo inarejesha hadhi yake ya Kitaaluma.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, akipokelewa na makamanda wa vikosi vya (14 na 151 KJ) wakati akiwasili katika kambi ya jeshi ya Ali Khamis Camp Vitongoji, kuangalia maendeleo ya shule ya msingi iliyo chini ya Jeshi hilo.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, akipokelewa na makamanda wa vikosi vya (14 na 151 KJ) wakati akiwasili katika kambi ya jeshi ya Ali Khamis Camp Vitongoji, kuangalia maendeleo ya skuli ya msingi iliyo chini ya Jeshi hilo.
Matengenezo hayo makubwa ya shule hiyo, nyumba za walimu na mabweni ya wanafunzi, pamoja na ujenzi mpya wa jengo la utawala na vyumba vya kusomea, yamegharimu zaidi ya shilingi Bilioni tatu na nusu.
Aidha katika hali siyokuwa ya kawaida, Maalim Seif aliingia madarasani kuona jinsi walimu wanavyofundisha pamoja na kuangalia ufahamu wa wanafunzi katika shule za Madungu na Fidel Castro
CHANZO MZALENDO.

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa