Home » » SMZ /ZMC Yaondosha Kituo cha Dala Dala Darajani

SMZ /ZMC Yaondosha Kituo cha Dala Dala Darajani

Kumekuwa na mtafaruk mkubwa leo hapa maeneo ya mjini na vitongoji vyake kufuatia uamuzi wa Baraza na Mji la Zanzibar (ZMC) na SMZ yake kuamua kuondosha kituo cha dala dala pale Darajani.
Wameyafanya haya bila kumshauri mtu, si wenye dala dala au wananchi watumiaji.
Yametangazwa haya kupitia ‘press conference’. Mkurugenzi wa Baraza la Mji (ZMC) Maalim Abeid Juma Kombo anaona inatosha kufanya hivyo. Wrong.Ilikuwa ZMC wakutane na stakeholders na isiwe leo kwa kesho!
ZMC, SMZ wanaona inatosha kuweka askari na bunduki pale Darajani kutisha watu na kuwapiga watu wanaopita eti wanavunja ‘kanuni’. Uamuzi huu umepata baraka zote za serikali, akiwemo Rais Shein, na CCM Zanzibar. Uamuzi huu wanaona unawakomoa wenye daladala, na wenyewe wanasema ‘wapemba’…..hizi ndio sera zao.
Ukweli hasa uamuzi huu unawasumbua sana wananchi wa Zanzibar, kuna walemavu, kuna wazee wasiojiweza, kuna wanafunzi wa skuli (wengine tayari wameanza kupotea) maana vituo vipya hawavijui, na in fact, havipo.
Uamuzi huu utaleta mvurugano mkubwa katika mji, uchafuzi wa mji, uvurugaji wa mipango miji.
Leo Mkurugenzi Abeid na Waziri wake Haji Omar Kheir anadhani kuweka kituo cha dala dala pale nyuma ya iliyokuwa baraza la wawakilishi la zamani, ni sawa. This is wrong, tena wrong sana.
Inanishangaza sana kuona uamuzi kama huu umefikiwa na aina ya watendaji tulionao leo, wamesoma, wametembea na kuona mambo: lakini ujinga, na kutu katika vichwa vyao umeganda, kama gundi.
Najua kuwa uamuzi huu unalenga zaidi kuelekea uchaguzi wa 2015, mipango hii inajulikana; ni mipango ya CCM na taasisi zake. Tayari kuna agenda nyingi zinagusa kuelekea uchaguzi — kupandisha kodi za utoaji wa makontena, kusajili wapiga kura feki (Pemba mpaka mtoto anayenyonya anaandikishwa — ah ziara ya makamo wa pili wa riais hiyo, Pemba juzi). na mengine mengi, kuajiri askari wengi wa vikosi hasa KMKM na baadaye kuwafukuza kazi, na baadaye hawa hawa wanakuwa majambazi!!
Hili na mengine yatajitokeza na tutayaona, lakini wanaoumia ni wananchi wote. Hili la kuhamisha vituo vya dala dala, Dr.Shein liangalie upya Dr. weeee; unachezewa akili na akina Abeid au kwa sababu jamaa yako wa Chokochoko/Mkanyageni na Mjimbini? Haya twendeni hivyo hivyo kijamaa jamaa na kujitegemea!
CHANZO;MZALENDO

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa