Home » » MWAPE SACCOS WAUNDA KAMATI KUBANA WADAIWA SUGU

MWAPE SACCOS WAUNDA KAMATI KUBANA WADAIWA SUGU

Wanachama wa MWAPE SACCOS wameunda kamati ya watu saba na kuipa jukumu la kufuatilia wadaiwa sugu walioshindwa kurejesha mikopo ambayo inafikia zaidi ya shilingi milioni 40.

Uamuzi wa kuunda kamati hiyo umefikiwa na wanachama wa Saccos hiyo kwenye mkutano wa dharura uliofanyika kwenye ukumbi wa Jamhuri na kuhudhuriwa na Mrajis wa Vya vya Ushirika Pemba Abdi Saleh wenye lengo la kutafuta njia ya kurejeshwa kwa mikopo hiyo .

Kamati hiyo inapongozwa na mwenyekiti Juma Shaban Juma ambapo Khamis Hamad Nassor ambayo imepewa jukumu la kukutana na wadaiwa sugu pamoja na wadhamini wa wadaiwa hao.

Mapema akitoa taarifa ya fedha , Mhasibu wa Saccos hiyo Rashid Said Nassor amesema kuwa kwa mujibu wa makubaliano mdaiwa anatakiwa kuwasilisha deni lake kila tarehe 12 ya kila mwezi.

Ameeleza kwamba Saccos inatakiwa kurejesha shilingi milioni 14, 835,000 /= kila mwezi katika benki ya CRDB , baada yab kukopeshwa shilingi milioni 300/= na hadi sasa wamefanikiwa kurejesha shilingi milioni 148,350,000/=.

Aidha amefahamisha kwamba hesabu hiyo ni ya marejesho 10 na wanatakiwa kurejesha marejesho 13 ili kufikia marejesho hayo bado wanadeni la shilingi milioni 44,505,000/=na kuongeza kuwa wana deni la shilingi milioni 151,650 ,000/= bila ya faida.

Kwa upande wake Mrajis wa vyama vya Ushirika Pemba, Abdi Saleh amewataka  viongozi wa Saccos hiyo kuandaa utaratibu utaofanikisha kurejeshwa kwa fedha za mikopo zilizoganda kwa wanachama .

Amesema kuwa MWAPE SACCOS ni moja ya Saccos ambazo malengo na mwelekeo wake ni mzuri, hivyo haitakuwa jambo la busara kuona kuwa wanachama wanashindwa kurejesha mikopo kwa wakati .



0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa