Home » » RAIA WA NCHINI ITALIA AFARIKI DUNIA AKIOGELEA

RAIA WA NCHINI ITALIA AFARIKI DUNIA AKIOGELEA

RAIA wa Italia, Caborn Michael (35), amefariki dunia katika bahari ya Matemwe mkoa wa Kaskazini Unguja, wakati akiogelea akiwa na chombo baada ya kupigwa na mawimbi.
Mwili wa marehemy ulifikishwa hospitali ya Mnazimmoja kwa uchunguzi.
Akithibitisha tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Hassan Muhammed Masangi, alisema, marehemu ambae alikuwa mtalii, alifikia hoteli ya Waridi iliyopo Matemwe tangu Januari 22 akiwa pamoja na mkewe alietajwa kwa jina la Monica Bars.
Alisema mwili wake ulipatikana Januari 28 katika ufukwe wa  hoteli ya Mapenzi Village iliyopo Pwani Mchangani na chombo alichokuwa akitumia kiliokotwa Kiwengwa.
Aliwataka watumiaji wa bahari kuwa waangalifu hasa katika kipindi hichi cha upepo.
Chanzo;Zanzinewz

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa