Home » » Wakulima waidai SMZ mil.240/

Wakulima waidai SMZ mil.240/

Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeombwa kuipatia fedha Wizara ya Kilimo na Maliasili kwa ajili ya kulipa deni wanazodaiwa na wakulima wa mpunga.
Akiwasilisha ripoti ya Kamati ya Fedha Biashara na Kilimo, Mwenyikiti wa Kamati hiyo, Salmin Awadh Salmin alisema wizara hiyo inadaiwa Sh milioni 240 na wakulima.
Alisema wakulima hao wanadai fedha hizo zaidi ya miezi minne, hali inayosababisha kurudisha nyuma maendeleo ya kilimo hicho na kukosa kujikimu kimaisha.
"Kamati ilielezwa kuwa wakulima wa mikataba wanaozalisha mbegu za mpunga katika mabonde mbalimbali wanaidai Wizara jumla ya Sh milioni 240 baada ya Wizara kuchukua mpunga huo bila ya kuwalipa kwa zaidi ya miezi minne ambapo wakulima wa bonde la Mtwango pekee wanadai Sh milioni 60," alisema.
Alisema tatizo hilo linaweza kuathiri uzalishaji wa mbegu hizo za mpunga, kitendo ambacho kinawavunja moyo wakulima na kuathiri kilimo hicho.
Salmin ametaka wizara hiyo ya Kilimo na Maliasili kupatia Chuo cha Kilimo kilichoko Kizimbani, mtaalam wa maabara ya mifugo na ulinzi wa uhakika ili kiweze kufanya
Chanzo;habari Leo

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa