Home » » Waangalizi, wasimamizi wadai zoezi la uchaguzi lilienda vizuri Unguja

Waangalizi, wasimamizi wadai zoezi la uchaguzi lilienda vizuri Unguja

.Wasimamizi wa Uchaguzi na waangalizi wa vyama  vya siasa wamesema, zoezi la uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki limekwenda vizuri licha ya kasoro iliojitokeza ya baadhi ya watu kutoona majina yao katika orodha ya matangazo ya wapiga kura yaliyobandikwa katika vituo siku 21 kabla ya kufanyika kwa uchaguzi huo.
Wakizungumza na Mwananchi wasimamizi hao,waangalizi wa ndani walisema vituo vilifunguliwa kwa wakati,vifaa vilifika mapema na hadi mchana hakukuwa na malalamiko yoyote katika zoezi hilo la upigaji kura linaloendelea.
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Uchaguzi Kiembesamaki, Suluhu Ali Rashid amesema,hadi mchana  zoezi la upigaji kura lilikuwa likiendelea vyema na hakukuwa na malalamiko ya watu kunyimwa haki ya kupiga kura kidemokrasia katika vituo vya uchaguzi.
Suluhu amesema, amepokea lalamiko moja la maneno kutoka kwa Mgombea wa Cuf, Abdulmalik Haji Jecha kuwa mawakala wake hawaridhiki na ukaguzi unaotumika kabla ya kupiga kura kama sheria inavyoelekeza, wakitaka shahada ya mpiga kura ikaguliwe na mawakala wa vyama kabla ya kuruhusiwa badala ya kutangaza jina na kuangaliwa katika daftari la wapiga kura.
  Alisema kwa mujibu wa sheria ya Tume ya Uchaguzi jina la mpiga kura linatakiwa kutangazwa na ofisa wa kituo na mawakala wa vyama kuangalia jina na picha yake katika orodha ya wapiga kura na si vinginevyo.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa