Home » » Zanzibar yapata sarafu maalumu ya mapinduzi

Zanzibar yapata sarafu maalumu ya mapinduzi

Zanzibar. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein jana amepokea rasmi Sarafu ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar huko katika Viwanja vya Maonesho ya Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar-SUZA Kampasi ya Beit el Ras.
Hafla hiyo ambayo ilikwenda sambamba na ufunguzi wa maonesho hayo ilishuhudiwa na Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad na Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi ambao nao walikabidhiwa sarafu hizo.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa sarafu hiyo na Naibu Gavana wa Benki Kuu, Juma Reli, Rais  aliupongeza uamuzi wa Benki Kuu wa kutoa sarafu hiyo maalum.
Alisema uamuzi huo ni wa kimaendeleo na kubainisha kuwa yeye na viongozi wenzake wanathamini sana sarafu hiyo, hivyo hawatakuwa tayari kuiuza hata kama thamani yake itapanda.
Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Gavana Juma Reli alieleza kuwa kukabidhiwa kwa sarafu hiyo kwa Rais kunaashiria uzinduzi rasmi wa uuzaji wa sarafu hiyo katika matawi yote ya Benki Kuu nchini.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa