Home » » Kuvamiwa watalii kwatia doa Zanzibar

Kuvamiwa watalii kwatia doa Zanzibar

Katibu Mkuu wa Tume ya Utalii Zanzibar, Salehe Ramadhani Ferouz, amesema mashambulizi ya baadhi ya watalii waliowahi kutembelea visiwa vya Zanzibar, yameifanya picha ya kisiwa hicho cha amani kubadilika.
Akizungumza na Mwananchi Jumapili Mjini Zanzibar, Ferouz alisema mashambulizi hayo yalikuwa mabaya na yalichafua mfumo mzuri uliojengwa kwa kipindi kirefu katika visiwa hivyo, na kwamba yamerudisha nyuma juhudi za tume ya kukuza utalii ndani ya Visiwa vya Zanzibar.
“Kama tume, tuna wakati mgumu sana kwa sasa, japokuwa wageni katika tamasha hili la Sauti za Busara wamekuwa ni wengi, lakini tuna imani mwaka huu idadi ingekuwa kubwa zaidi, vitendo hivi ndivyo vinatukwamisha,” alisema.
Kwa mujibu wa ofisa huyo wa utalii wa Zanzibar, amesema kuwa wamekuwa wakikusanya wageni wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani, tangu kuanzisha kwa tamasha hilo kwa mara ya kwanza miaka 11 iliyopita.
“Tunapata ahueni kubwa ya watalii wakati wa tamasha hili linalochukua muda wa siku nne, hoteli zote hapa mjini zimejaa, hii yote ni katika utalii wa muziki kwani wengi zaidi wanapendelea kuja msimu huu kushuhudia tamasha la muziki wa asili,” alisema Ferouz.
Kwa mujibu wa Ferouz, utalii ni sekta inayoongoza katika kukuza uchumi Zanzibar kwnai inachangia asiliamia 25 ya Pato la Taifa (GDP) na asilimia 80 ya ukusanyaji wa kodi za serikali.
Mwishoni mwa mwaka jana , Zanzibar ilikuwa inakabiliwa na mashambulizi ya tindikali, ambayo wanawake wawili kutoka Uingereza Katie Gee na Kirstie Trup, wote wakiwa na umri wa miaka 18, wakati wakitembea katika njia ya sehemu ya zamani ya mji mkuu wa Zanzibar, walimwagiwa tindikali na watu wawili waliokuwa wakiendesha pikipiki.
Mashambulizi ya hivi karibuni yakiwamo ya upotevu wa wanandoa wa Kifaransa ambao wanaaminiwa kwamba waliuawa na kutupwa katika kisilinalozunguka nyumba yao.
Francois Cherer Robert Daniel na Brigette Mery walionekana kwa mara ya mwisho mwaka jana. Taarifa kwamba wamepotea zilianza kutangazwa Desemba 27 mwaka jana.
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa