Home » » Sauti za Busara ni zaidi ya tamasha

Sauti za Busara ni zaidi ya tamasha

Siku nne zimesalia kabla ya siku nne za kuandika historia nyingine Visiwani Zanzibar kupitia onyesho kubwa la sanaa na muziki la kimataifa linalotambulika kwa jina la Sauti za Busara.
Tamasha hilo lilianzishwa miaka 11 iliyopita na kufanyika kila mwaka, linatarajiwa kuanza Februari 13 na kuhitimishwa tarehe 16 ya mwezi huu.
Sauti za Busara ni tamasha linalowakutanisha wasanii wa Kiafrika ili kuutangaza, kuhamasisha na kusherehekea utamaduni wao bila kusahau wageni kutoka mataifa mbalimbali duniani ambao pia hufika kushuhudia na hata kushiriki.
Kupitia tamasha hilo wasanii hupata fursa ya kujitangaza kimataifa wao binafsi au vikundi vyao hata kufanikiwa kuvuka anga na kutambulika ndani na nje ya Bara la Afrika.
Baadhi ya wasanii waliofanikiwa kuvuka anga za kimataifa kupitia Tamasha la Sauti za Busara ni pamoja na Jhikoman, Abantu Mandingo, Mrisho Mpoto.
Hata hivyo, mbali ya kusherehekea utamaduni wa Kiafrika tamasha hilo lina faida nyingine zinazojitokeza kwa wasanii.
Mwenyekiti wa Bodi ya Tamasha la Sauti za Busara, Samia Mohamed anaeleza kuwa kila mwaka tamasha hilo limekuwa likitoa ajira kwa zaidi ya Watanzania 150 jambo alilosema siyo rahisi kufikiriwa au kufahamika na Watanzania wengi.
Mbali na ajira, Mohamed anasema kuwa tamasha hilo pia limekuwa likikuza vipaji vya muziki kupitia kitengo chake kijulikanacho kwa jila la ‘Busara extra’.
 “Hatua hiyo inafanyika kwa kujumuisha matukio mbalimbali ya maonyesho ambayo hutoa fursa kwa wasanii wa ndani kuonyesha kazi zao binafsi,” anasema na kuongeza;
“Hatua hiyo imekuwa ikishawishi ongezeko la watalii wanaotembelea sehemu mbalimbali za utalii Visiwani Zanzibar.
Hali itakavyokuwa
Katika msimu wa Sauti za Busara, miji ya Zanzibar hufurika wageni kutoka mataifa mbalimbali kutoka Afrika Mashariki, Magharibi, Kaskazini, Kusini na nje ya bara hilo, huku biashara ya utalii ikiongezeka kwa kasi.
Hadi sasa, mataifa mbalimbali duniani yameanza kuelekeza macho na masikio yake Visiwani Zanzibar tayari kushuhudia tamasha hilo kwa msimu wa mwaka huu 2014.
Baadhi ya shughuli zinazotarajiwa kutangulia mjini Zanzibar katika uzinduzi wa tamasha hilo ni pamoja na maonyesho ya filamu za Kiafrika, Kongamano la Wataalamu wa Filamu sanjari na paredi maalumu siku ya ufunguzi wa Tamasha la Busara.
Mohamed anasema kuwa tamasha hilo halitakuwa na mgeni rasmi, badala yake Watanzania wote na Waafrika wote watahusika.
“Tangu tumeanza tamasha hili, miaka yote hatujawahi kuwa na mgeni rasmi anayepewa kipaumbele tofauti na Watanzania wenyewe lengo likiwa  kutoa  nafasi sawa ya kujionea fahari ya tamasha hilo,” anasema.
Tofauti ya msimu huu
Mohamed anasema kuwa kwa mwaka huu tamasha hilo linatarajiwa kuwa tofauti likilinganishwa na miaka iliyopita kutokana na kuongezeka kwa maboresho mbalimbali ikiwamo ushiriki wa mataifa ya Magharibi.
 “Pia hata ubora wa wasanii watakaoshiriki, ulinzi, ubora wa vyombo vya muziki pamoja na vitu vingine vingi,” anasema Mohamed. Anabainisha kuwa pia Tamasha la Sauti za Busara msimu huu litashuhudia  uzinduzi wa mradi mpya ujulikanao kwa jina la ‘Santuri safari’ ukiwa na dhamira ya kuangalia jukumu la MaDJ katika ukuzaji wa muziki wa Afrika Mashariki.
“MaDJ waalikwa, wazalishaji wa muziki, watalaamu wa sauti, waandaaji wa matamasha na wataalamu wa sanaa kutoka ukanda wa Afrika watajumuika pamoja Zanzibar na kupata mafunzo hayo. Hiyo itakuwa fursa muhimu  katika kuangalia vitu vya kisasa,” anasema Mohamed.
Wasanii watakaoshiriki
Jumla ya vikundi 32 ndivyo vitakavyoshiriki Sauti za Busara na kushambulia jukwaa ‘live’  vikichujwa kutoka vikundi 560 vilivyoomba kushiriki, huku 135 kati ya hivyo vikitoka Tanzania.
Baadhi ya vikundi na wasanii wataoshiriki ni pamoja na Tausi Women’s Taarab (Zanzibar) Seven Survivor (Tanzania), Baladna Taarab (Zanzibar) na  Kundi la Jupiter, Okwess International (DRC).
Wengine ni Dizu Plaatjies na The Ibuyambo Ensemble ( Africa Kusini), Addis Acoustic Project ft Melaku Belay (Ethiopia), OY (Ghana), Switzerland Street Rat and Body Mind Soul (Malawi) na  Majestad Negra (Puerto Rico).      
Hadi sasa, mataifa mbalimbali duniani yameanza kuelekeza macho na masikio yake Visiwani Zanzibar tayari kushuhudia tamasha hilo kwa msimu wa mwaka huu 2014.
Baadhi ya shughuli zinazotarajiwa kutangulia mjini Zanzibar katika uzinduzi wa tamasha hilo ni pamoja na maonyesho ya filamu za Kiafrika, Kongamano la Wataalamu wa Filamu sanjari na paredi maalumu siku ya ufunguzi wa Tamasha la Busara.
Mohamed anasema kuwa tamasha hilo halitakuwa na mgeni rasmi, badala yake Watanzania wote na Waafrika wote watahusika.
“Tangu tumeanza tamasha hili, miaka yote hatujawahi kuwa na mgeni rasmi anayepewa kipaumbele tofauti na Watanzania wenyewe lengo likiwa  kutoa  nafasi sawa ya kujionea fahari ya tamasha hilo,” anasema.
Wamo pia Jhikoman (Tanzania) Hoko Roro (Tanzania) Ashimba (Tanzania, Finland) Swahili Vibes (Zanzibar), Tritonik (Mauritius) Joel Sebunjo (Uganda), Abantu Mandingo (Tanzania), Segere Original (Tanzania), Moyize (Rwanda) na Ricky na Marafiki (Kenya). 
 
Tamasha bila Bi Kidude
Kwa mara kwanza tamasha hilo linafanyika bila kuwepo kwa mwanamziki mkongwe na mashuhuri aliyeacha historia na heshima kubwa ya kipekee, marehemu Bi Kidude.
Hata hivyo, Mohamed anasema kuwa hadi sasa wamezungumza na Baraza la Sanaa Visiwani humo na taasisi mbalimbali kwa ajili ya kuandaa mpango wa kumuenzi Bi Kidude.
“Suala hilo tumewaachia Baraza la Sanaa, ila sisi tutabaki kama washauri kuhakikisha kunakuwa na hatua fulani ya kumuenzi katika miaka yote aliyoshiriki katika muziki enzi za uhai wake,” anasema Mohamed.

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa