Makontena sita yaliyobeba magogo yaliyokuwa yakisafirishwa
kwenda nje kwa njia za magendo yamekamatwa katika Bandari ya Malindi,
Kisiwani Unguja kabla ya kusafirishwa kuelekea nchini China, imefahamika
visiwani humu.
Akizungumza na gazeti hili jana, Meneja wa
Operesheni ya Mamlaka ya Kodi ya Mapato Tanzania (TRA) Kanda ya
Zanzibar, Ali Bakari amethibitisha makontena hayo kuzuiwa. Uchunguzi
umeanza kufanyika baada ya kubainika kuwa yamesafirishwa kinyume na
sheria yakitokea nchini Madagascar.
Bakari alisema chimbuko la kukamatwa kwa makontena
hayo kumetokana na taarifa zilizotolewa na Shirikisho la Huduma za
Forodha Duniani, (WCO) kwamba kuna meli zinazobeba magogo kutoka
Madagascar na kupitishwa katika mwambo wa Tanzania na Kenya.
Meneja huyo alisema taarifa hizo zilieleza kuwa
matukio hayo yangetokea kati ya Agosti na Februari mwaka jana na mwaka
huu katika mwambao wa Tanzania. Baada ya kuanza kufuatilia ikabainika
kuanza kujitokeza kwa meli ndogo ndogo zikishusha magogo Visiwani
Zanzibar.
Hata hivyo, hakuwa tayari kutaja jina la kampuni
inayomiliki magogo hayo na kuitumia Kampuni ya Wakala wa Mizigo ya
Visiwani Enterprises kusafirisha mzigo huo .
Kuhusu sakata hilo, Mkurugenzi wa Idara ya Misitu
na Maliasili, Sheha Idrisa Hamdan alithibitisha kuingizwa kwa shehena ya
magogo Zanzibar zikitokea Madagascar.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment