Home » » Magogo ya magendo sasa kurudishwa

Magogo ya magendo sasa kurudishwa

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, imesema shehena ya magogo yaliyokamatwa yakiingizwa nchini kwa njia ya magendo yakitokea Madagascar yatarejeshwa nchini humo, kwa sababu Zanzibar haina sheria ya misitu ya kuwashtaki au kutaifisha shehena aina hiyo.
Akizungumza na Mwananchi ofisini kwake Darajani mjini Unguja, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo na Maliasili, Dk Bakari Asseid, amesema Sheria ya Misitu na Maliasili ya mwaka 1996 haizungumzii rasilimali za misitu zinazokamatwa kutoka nje ya nchi na kupitia Zanzibar.
Dk Assweid alisema wizara yake imepewa uwezo wa kukamata mzigo wa aina hiyo na kuurejesha mahali ulikotoka lakini haina uwezo wa kuwakamata wahusika na kuwafungulia mashtaka mahakamani.
Alisema sheria ya kimataifa ya kulinda misitu na wanyamapori, walioko katika hatari ya kutoweka imeridhiwa na kusainiwa na Tanzania, lakini ikiwa haijaridhiwa na Zanzibar.
Pia alisema mambo ya kilimo na maliasili hayamo katika orodha ya mambo ya Muungano kwamba maazimio na sheria za kimataifa zinazopitishwa hazijawa na mamlaka ya kufanyakazi Zanzibar.
“Mamlaka ya dhamana tumeshazipa maelekezo ya kutosha kwa mujibu wa sheria, magogo hayo yanapaswa kurejesha wa mahali yanakotoka mara moja, hatuna sheria ya kuwashtaki au kutaifisha mzigo huo, suala hilo liko nje ya uwezo wetu kisheria,” alisema Dk Asseid.
Pia alikiri kuwa Bandari ya Malindi kuanzia Desemba mwaka jana, imekuwa ikisafirisha kiwango kikubwa cha shehena ya magogo.
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa