Home » » Watalii kupungua Zanzibar

Watalii kupungua Zanzibar

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Watalii kupungua ZanzibarKAMPUNI inayojishughulisha na kupokea watalii imesema  hali ya kuwepo milipuko ya mabomu mara kwa mara katika visiwa vya Zanzibar inaweza kuchangia kupungua kwa watalii katika visiwa hivyo iwapo hali hiyo haitadhibitiwa.
Siku mbili zilizopita ilitokea milipuko minne inayoaminika kuwa ni mabomu katika maeneo matatu tofauti katika visiwa vya Zanzibar na watu wanne kujeruhiwa.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mkurugenzi wa kampuni mmoja ya utalii nchini, Masque Herriton, alisema wamekuwa wakipokea simu kutoka nchi mbalimbali ambazo zimetaka kujua juu  ya hali za wananchi wao.
“Tuna siku mbili tunapokea simu kutoka mataifa mbalimbali, ambapo wanahitaji kujua kuhusu wananchi wao walioingia kupitia kampuni yetu kama wapo salama,” alisema.
Herriton alisema kuna haja ya serikali kuangalia namna ya kupunguza ama kutokomeza matukio hayo Zanzibar kwa kuwa inaweza kuleta athari kiuchumi.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa