Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kutoka Zanzibar wamejipanga
ili kuwashawishi wajumbe wengine wakubali pendekezo la kuiongezea
Zanzibar, mgawo wa mapato ya Muungano.
Mmoja wa wajumbe hao, Juma Ali Khatibu alisema
Zanzibar inapaswa kuongezewa mgawo kutoka asilimia 4.5 ya sasa hadi
kufikia asilimia 20.
“Zanzibar tulisema kuwa hatunufaiki na ajira za
Serikali ya Muungano lakini hilo limetatuliwa na sasa tunataka
tuongezewe mgawo wa mapato,” alisema Khatibu.
Akimnukuu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
(Menejimenti ya Utumishi wa Umma), Celina Kombani, Khatibu alisema
Wazanzibari wanapata asilimia 21 ya ajira kwenye taasisi za Muungano.
“Kwa hiyo kupitia Bunge hili, mimi nilikuwa
nawaomba Wazanzibari wenzangu tuitetee Zanzibar hasa kwenye ile asilimia
4.5 ya mgawanyo wa mapato,” alisema.
“Wakati ule tulikuwa 300,000, siku hizi tumekuwa
wengi. Hapa ndiyo mahali pa kuomba mgawo uongezeke kutoka asilimia 4.5
hadi angalau 20 au 21 hivi,” alisisitiza.
Kauli hiyo iliungwa mkono na Waziri wa Nchi katika
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Abood, ambaye
alisema mgawanyo wa mapato ya Muungano ni jambo linalopaswa kuzungumzwa
kwa kina.
“Ni jambo kubwa sana linalohitaji kuzungumzwa kwa
kina katika Bunge letu hili. Ukiondoa tatizo hili manung’uniko yote
yatakuwa yamekwisha,” alisema Abood.
Abood ambaye pia ni mjumbe wa Bunge hilo, alisema
kimeanzishwa chombo cha kusimamia masuala ya fedha kwa pande mbili za
Muungano.
“Wazanzibari wapate fursa iliyo sawa na Bara. Tutengeneze msingi utakaotengeneza usawa katika mgawanyo wa mapato,” alisisitiza.
Waziri huyo alisema suala la Zanzibar kuongezewa
kiwango cha mgawo linazungumzika katika Bunge Maalumu la Katiba, kama
kutakuwa na dhamira njema.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment