Home » » KIKAO CHA BAJETI YA ZANZIBAR LEO

KIKAO CHA BAJETI YA ZANZIBAR LEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Kikao cha majadiliano ya Bajeti ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2014/2015 kitaaza leo katika Baraza la Wawakilishi kisiwani hapa, miswada miwili ya sheria itawasilishwa na kujadiliwa.
Hayo yalielezwa na Katibu wa Baraza hilo, Yahya Khamis Hamad alipozungumza na waandishi wa habari kwa lengo kueleza shughuli za kikao hicho huko Mbweni nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Hamad aliitaja miswada hiyo kuwa ni ule wa Sheria ya Fedha pamoja na wa Sheria ya kuidhinisha matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2014/2015.
Alifafanua kuwa mswada wa fedha ukishapitishwa ndiyo utakaotoa mwelekeo wa matumizi ya bajeti hiyo kuazia Julai mosi mwaka huu na kuiruhusu SMZ kutumia kiasi cha fedha kilichoidhinishwa.
“Ni imani yangu kwamba miswada hiyo itapitishwa bila vikwazo ili kuruhusu Serikali kuendesha shughuli zake” alisema katibu huyo.
Pia katibu huyo alieleza mbali na shughuli hizo katika kikao hicho cha 16 ndani ya baraza la tano, maswali 90 yataulizwa na kujibiwa.
Alisema kwa mara ya kwanza kikao cha bajeti, kitaweza kupokea uwasilishwaji wa mpango wa maendeleo ya Zanzibar wakati wa asubuhi na jioni waziri wa fedha atawasilisha Makadirio na Matumizi ya Serikali.
Katibu huyo aliwaonya wajumbe wa baraza hilo, wasihusishe Bunge la Katiba na kikao hicho, ili kuepusha malumbano.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa