Home » » TTCL YAZIDI KUJIIMARISHA PEMBA

TTCL YAZIDI KUJIIMARISHA PEMBA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KAMPUNI ya mawasiliano Tanzania (TTCL) imeanza ujenzi wa ofisi ya kisasa ya huduma kwa wateja katika eno la Madungu, Chakechake, Pemba itakayogharimu sh bilioni 1.2.
Akizungumza  na waandishi wa habari visiwani Pemba hivi karibuni kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura, Mkuu wa Kitengo cha Ufundi, Mtandao na Ukarabati, Jothan Lujara, alisema kampuni yao inaanza ujenzi katika eneo hilo kama njia ya kujiimarisha katika utoaji huduma visiwani hapa na nchi nzima kwa ujumla.
“Kwa muda mrefu, tulikuwa tukitoa huduma zetu kwa wateja kwa kutumia jengo la kukodi katika eneo hili, na sasa tumeamua tuwe na jengo letu,” alisema.
Alisema kati ya fedha hizo, sh bilioni 1.1 atalipwa mkandarasi atakayejenga jengo hilo na na sh milioni 93 atalipwa mshauri mwelekezi wa ujenzi.
“Fedha zote hizi zinagharimiwa na kampuni yetu kutokana na vyanzo vyake vya mapato,” alisema na kuongeza kuwa jengo hilo litakuwa na ghorofa moja.
Alisema jengo hilo linatarajiwa kujengwa katika kipindi cha miezi nane na kukamilika Februari mwakani.
Mkuu wa Mkoa Kusini Pemba, Juma Kasim Tindwa, alisema jengo hilo litasaidia kutoa huduma nzuri Chakechake kwa vile linajengwa kisasa na lenye nafasi kubwa.
“Leo naikabidhi Kampuni ya MS Quality Building Contractors Ltd ili ianze rasmi ujenzi huu na matarajio yangu itamaliza kwa wakati,” alisema.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Blogs za Mikoa Tanzania
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Blogs za Miikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa