Home » » MPANGO WA AJIRA ZA MUDA KWA WALENGWA WA KAYA MASKINI CHINI YA TASAF WASHIKA KASI KISIWANI ZANZIBAR.

MPANGO WA AJIRA ZA MUDA KWA WALENGWA WA KAYA MASKINI CHINI YA TASAF WASHIKA KASI KISIWANI ZANZIBAR.


Wakazi wa kijiji cha Mzuri -Makunduchi mkoa wa Kusini Unguja wakiwa katika mradi wa kitalu cha miti moja ya mradi ulioibuliwa na walengwa wenyewe kupitia PWP unaoendeshwa na TASAF ambapo walengwa hulipwa fedha kwa kazi hiyo.
Kitalu cha miti kilichotayarishwa na walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini kupitia mpango wa ajira za muda wa TASAF wenye lengo la kuwaongezea kipato kwa kuwalipa kulingana na ushiriki wao katika kazi hiyo.
Walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini  unaotekelezwa na TASAF wakishiriki katika kazi za kutayarisha kitalu cha miche ya miti katika kijiji cha Mzuri -Makunduchi mkoa wa Kusini Unguja.
Mfuko ya miche ya miti iliyotayarishwa na wakazi wa kijiji cha Mzuri Makunduchi mkoa wa Kusini Unguja wakishiriki katika kazi ya kujaza udongo ikiwa ni utekelezaji wa Mpango wa ajira za muda PWP unaotekelezwa na TASAF.

Kazi ya ujenzi wa barabara katika kijiji cha Kijini -Makunduchi mkoa wa kusini Unguja ambayo ni moja ya mkakati wa TASAF wa kuwaongezea kipato walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini kupitia ajira ya muda PWP.
Baadhi ya walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini unaotekelezwa na TASAF katika kijiji cha Kijini Makunduchi mkoa wa kusini Unguja wakishiriki katika kazi za ujenzi wa barabara kupitia mpango wa ajira za muda PWP.
Walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini katika eneo la Kijini Makunduchi mkoa wa kusini Unguja wakiwa katika harakati za ujenzi wa barabara kupitia mpango wa ajira za muda PWP kupitia TASAF.
Barabara inayojengwa kupitia mpango wa ajira ya muda PWP ambapo walengwa wa Mpango wa Kunusuru kaya maskini kupitia TASAF wakiwa katika eneo la mradi wa barabara yenye urefu wa kilometa Moja .

Walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF wameanza utekelezaji wa miradi ya ajira za muda na kisha kulipwa ujira katika miradi wanayoibua kwenye maeneo yao .
Walengwa wa vijiji kadhaa vilivyoko kwenye Mpango huo kikiwemo kile cha Mzuri na Kijini vilivyoko katika eneo la Makunduchi mkoa wa Kusini Unguja wameanza kutengeneza barabara yenye urefu wa zaidi ya kilometa moja na vitalu vya miche ya miti ya asili na matunda katika eneo lao na kisha kulipwa fedha chini ya utaratibu ulioandaliwa na TASAF ambao ni moja ya mkakati  wa kuwaongezea kipato walengwa na kupambana na umaskini.

Akizungumza na timu ya waandishi wa habari waliotembelea eneo hilo Sheha wa eneo hilo Bwana Mwita Masemo Makungu amebainisha kuwa mpango huo umeitikiwa vizuri na walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini katika eneo hilo na kuwa jitihada hizo za TASAF zimeamsha ari ya wananchi kujiletea maendeleo kwenye maeneo yao na kupunguza kero ya barabara iliyokuwa inawakabili.

Hata hivyo Bwana Makungu amesema pamoja na ushiriki wa wananchi kwenye kazi hiyo kupitia mpango wa ajira za muda bado wananchi hao wanakabiliwa na tatizo la vifaa na utaalamu hususani katika ujenzi wa barabara ambao unahitaji vifaa vizito ambavyo havipo kwenye maeneo yao na hivyo kuomba serikali kuona namna ya kukamilisha kazi hiyo.

Zifuatazo ni baadhi ya picha za walengwa wa PSSN katika wilaya ya Makunduchi mkoa wa Kusini Unguja wakishiriki katika kazi kupitia ajira za muda PWP.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa