Home » » RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein jana aliungana pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba katika futari maalum aliyowaandalia

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein jana aliungana pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba katika futari maalum aliyowaandalia

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein jana aliungana pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba katika futari maalum aliyowaandalia, ikiwa ni miongoni mwa utamaduni anaouendeleza wa kufutari pamoja na wananchi wa Mikoa yote ya Zanzibar kila ufikapo mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Hafla hiyo ya futari ilifanyika katika viwanja vya Ikulu ndogo ya Chake Pemba, na kuhudhuriwa na wananchi pamoja na viongozi mbali mbali wa Mkoa huo pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali.

Aidha, Mama Mwanamwema Shein naye aliungana pamoja na akina mama wenzake wa Mkoa huo katika futari hiyo ya pamoja.

Mara baada ya futari hiyo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman Abdalla alitoa shukurani kwa wananchi pamoja na viongozi wote waliohudhuria katik muwaliko huo.

Kwa aniaba yake, familia na Serikali, alisisitiza kuendeleza ushirikiano na mshikamano uliopo kwani ushirikiano ndio nguvu ya kila kitu.

Sheikh Mohammed Suleiman kutoka  Masjid Al-Halil Cheke Chake, akitoa neno la shukurani kwa niaba ya wananchi hao waliofutarishwa na Alhaj Dk. Shein alitoa pongezi na shukurani kwa mwaliko huo wa Rais.

Katika shukurani hizo Sheikh Mohammed alitumia fursa hiyo kueleza furaha waliyokuwa nayo wananchi hao na kusisitiza kuwa  Alhaj  Dk. Shein anapaswa kupongezwa sana kutokana na mengi aliyowafanyia wananchi wa Zanzibar.

Sheikh Mohammed alimuelezea Alhaj Dk. Shein jinsi anavyoweza kukaa pamoja na wananchi na kuweza kushirikiana nao vizuri huku wakitoa shukurani kwa kuiongoza Zanzibar kwa amani na utulivu hadi leo hii.

Alise

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa