Home » » WANACCM na wananchi kisiwani Pemba wametakiwa kutotishika na vitisho vinavyotolewa na viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani

WANACCM na wananchi kisiwani Pemba wametakiwa kutotishika na vitisho vinavyotolewa na viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WANACCM na wananchi kisiwani Pemba wametakiwa kutotishika na vitisho vinavyotolewa na viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani vya kuwafanyia hujuma siku ya uchaguzi mkuu Oktoba 25 mwaka huu kwani vyombo vya ulinzi na usalama vimejiapanga kuwalinda katika kutekeleza haki yao hiyo ya kikatiba.

Wakizungumza katika nyakati tofauti katika mkutano wa Kampeni ya uchaguzi wa CCM uliofanyika Mtambwe leo, Mkoa wa Kaskazini Pemba, viongozi wa CCM waliohudhuria mkutano huo walisema vyama vya upinzani vimeshajua kuwa kuna kila dalili kwa CCCM kushinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi huu na kwamba njia pekee inayokusudiwa kufanywa na upinzani ni kutumia vitisho kwa lengo la kuwazuia wapiga kura wa CCM.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM ambaye pia ni Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi amesema Serikali imegundua mbinu zinazokusudiwa kufanywa na vyama vya upinzani na amewahakikishia wanaCCM na wananchi kwamba Serikali imejidhatiti kukabiliana na hali yoyote itakayojitokeza kwa kuweka ulinzi imara ili wananchi wote waweze kuitumia haki yao ya kuchagua viongozi wanaowataka.

Balozi Seif Ali Iddi aliwataka wananchi wa Mtambwe kuwa makini kusikiliza sera za wagombea kutoka vyama mbali mbali vya siasa lakini kuwachagua wagombea wa CCM ambao ahadi zao zinatekelezeka.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, alishangazwa na kauli za baadhi ya wagombea wenye kunadi maendeleo kwa wapiga kura wakati wao wenyewe wameshindwa kuonesha mfano kwenye vijiji walivyotoka licha ya kuweko madarakani kwa muda mrefu.

Viongozi wa CCM waliopata fursa ya kusalimiana na wananchi pamoja na WanaCCM waliohudhuria katika mkutano huo walielezea kuridhishwa kwao na hali ya mabadiliko na ukuaji wa demokrasia na maendeleo katika jimbo la Mtambwe ambako wananchi wameonesha kuwa huru kuchagua sera za chama wakipendacho wakionesha mabango yanayosomeka "kubadili chama siyo kurtadi".

Alieleza kuwa wimbi kubwa limekuwa linaikimbia CUF na kuipongeza wanaMtambe walio wengi kujiunga na CCM na kuendelea kukiunga mkono kwa nguvu zao zote chama hicho cha CCM.

Akizungumzia maendeleo ya Mtambwe na Pemba kwa jumla, Balozi Seif Ali Iddi alisema kuwa miongoni mwa juhudi zilozofanywa na serikali ndani ya miaka mitano chini ya uongozi wa Dk. Shein ni hatua yake ya kulirejeshea hadhi yake zao la karafuu na kuwapa pencheni wazee waliotimia miaka 70.

Alisema kuwa Dk. Shein ameondosha gharama zilizokuwa zikilipwa na wazazi kaondosha na hivi sasa akina mama watakuwa wakipata huduma hizo bure ambapo pia hivi karibuni aliahidi kuwa akipewa ridhaa atatoa mshahara kima cha chini laki tatu kwani Dk. Shein hadanganyi na anatenda alichoahidi.

Aliwataka wananchi na wanaCCM kuangalia chama kinachotekeleza ahadi zake kwa wananchi huku akisisitiza kuwa ataendelea kuwa Mwakilishi wa Jimbo la Mahonda kwani anauhakika na ushindi hadi pale atakapoamua kupumzika.

Alisema kuwa mbinu zinafanywa ikiwa  ni pamoja na kununua vitambulisho vya CCM,  na kuwaambia kuwa hivi sasa viongozi wa upinzani wanawatisha wananchi kuwa CUF wakishindwa nyumba za wafiasi wa CCM watazichoma moto na kuwataka wananchi kutotishika. na kutokubali kutishwa.

Alisema kuwa vyombo vya ulinzi na usalama viko macho na kusisitiza kuwa ushindi wa CCM ni lazima mwaka huu, na kuwataka wanaCCM wa Pemba kupamba maskani zao, nyumba zao kwani ushindi kwa CCM hauepukiki.

Aliwataka wananchi kuamka mapema kwenda kupiga kura, na baadae kurudi nyumbani na kuwahakikishia wananchi kuwa kutakuwa na ulizni wa kutosha ili kila mwananchi apige kura kwa amani na utulivu.

Balozi Seif alitoa salamu kwa wananchi wa Kinyikani Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Jimbo la Kojani ambao wameamua kujitoa katika chama cha CUF na kujiunga na CCM kwa kuomba kujengewa barabara yao kutoka Mzambarauni hadi Mchangamdogo.

Nae Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohammed Aboud alisema kuwa katika kipindi cha miaka mitano Djk. Shein amefanya kazia mkubwa ya kuleta maelndeleo, na mfamo ni barabara kutoka Bahanasa kuja Mtambwe.

Alisema kuwa sio tu ujenzi wa barabara, bali ni kuhakikisha wananchi wa Unguja na Pemba wanapata mambo ya msingi ikiwa  ni pamoja na huduma za afya, elimu, maji, umeme, biashara na nyengine kwani amefanya kazi za maendeleo nchini hivyo kuna kila sababu ya kumpa kura za ndio Dk. Ali Mohamed Shein.

Waziri Mohammed alisema kuwa Dk. Shein ni hidaya kwa Zanzibar kwani ni mkweli, mchapa kazi, hana makuu, mwenye subira na mfano wa kuonesha kuwa ameweza kuhimili vituko vingi ambavyo vimefanywa na wapinzani ili kuvuruga amani ambapo Dk. Shein amejitahidi kuhakikisha hilo halitokei.

Alisema kuwa Dk. Shein ameshajenga misingi imarana na amejitahidi katika miaka mitano kwa kuijenga Zanzibar mpya sambamba na kufungua milango ya kuimarisha uwekezaji ili kuhakikisha uchumi unaimarika kwani nia yake ni kuondoa umasikini.

Alisema kuwa uchaguzi sio shwangwe na matusi bali uchaguzi ni takwimu, na tayari kwa upande wa takwimu CCM imejipanga vizru hivyo shangwe hizo ni kazi bure.

Alisema kuwa mara hii CCM haikubali kuibiwa kura zake kisiwani humo kama ilivyozoeleka na kusema kuwa mara hii CCM imejipanga kuhakikisha uporaji wa kura zao unadhibitiwa.

Wapo wafusi wa CUF ambao wameshajua kuwa CUF imeuzwa na wamesema hawakubali kwani chama hicho hakina Mgombea Mwenza.

Aidha, alieleza kuwa chama cha CUF kinajisifu kuwa tayari kimeshawapata ma PO na ma PC ambao watawasaidia katika kufanya vile watakavyowaamuru na kusema kuwa atakaejaribu kuiba kura hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Waziri Aboud alisema kuwa wafusi wa chama hicho cha upinzani wamekuwa wakijisifu kuwa mara hii watahakikisha wanaiba kura na kuitaka Tume ya Uchaguzi kulitambua jambo hilo ambalo ni njia moja wapo ya kuvuruga amani.

Alisema kuwa chama hicho kimejipanga kwa lengo la kuwa wamejipanga kuwa na Mawakala wengi ili kufanya uharibifu mara hii hakuna kugaiwa juisi, maji, pilau kwani mara hii CCM imejipanga vizuri kwa Mawakala wake.

Nae Balozi Amina Salum Ali alisema kuwa CCM itaendelea kuuonesha ulimwengu kuwa iko hai na itaendelea kuongoza taifa la Tanzania na kuwataka wanaCCM kuendelea kukiunga mkono chama chao hicho.

Alisema kuwa CUF haina itikadi wala Sera na kushangwazwa kama kweli hayo yapo basi maendeleo makubwa yangeweza kupatikana na kueleza kuwa kinachofanyika ni hadaa.

Alisema kuwa upinzani hawaelewi Utaifa kwani viongozi wa vyma vya upinzani hawawaelezi wananchi na wafuasi wao umuhimu wa Utaifa na badala yake huwatia kasumba kwa lengo la kuichukia Serikali yao.

Alisema kuwa maendeleo yanayotekelezwa na Dk. Shein ni kwa ajili ya wananchi wote na kuwaeleza kuwa hata viongozi wa upinzania wanajua kuwa hakuna maendeleo kama hakuna Sera.

CCM ndio chama pekee kinachoimarisha maendeleo, na kusema kuwa CCM inawajali wananachi wote wa Tanzania na Serikali zote mbili zimekuwa zikileta maendeleo kwa wananchi wote bila ya kuwabagua.

Kwa upande wa akina mama, Balozi amina alisema kuwa akina mama wa Mtambwe wana nguvu ya kuwashawishi akina baba kuiunga mkono CCM ili baadae wasije kujutia na kusisitiza kuwa Dk. Shein amekuwa akihakikisha kuwa maendeleo yanafikiwa na wananchi wote hapa Zanzibar.

Waziri wa Kilimo na Maliasili, Dk. Sira Ubwa Mwamboya alisema kuwa Mtambwe ya leo sio ile ya miaka mitano iliyopita kwani huduma zote muhimu zipo na kushangwazwa na kiongozi wao mkuu Edward KLowasa kudai kuwa akipata uongozi atapeleka elimu, afya na Mamlaka Kamili na kueleza kuwa hayao yote yapo yameshaletwa na CCM.

Aliwataka wananchi kuwapigia kura viongozi wote wanaogombania nafasi kwa upande wa CCM.

Nae Balozi Ali Karume ambaye pia ni Mjumbe wa Halmahsuri Kuu ya CCM aliwataka wanaCCM na  wananchi wa Mtambwe kuwapa kura viongozi wa CCM akiwemo Dk. Ali Mohamed Shein, Dk. Magufuli, Wabunge, Wawakilishi na Madiwani wa CCM.

Hakuna kitu ambacho unaweza kukitetea kama hukiamini hivyo alisisitiza kuwa ipo haja ya kumchagua Dk. Shein huku akieleza kuwa CCM ina historia kuwa tokea ASP katika suala la ushindi na mwaka huu CCM itaendelea kushinda.

Aliwataka wananchi wa Pemba kutoregeza kamba katika zao la karafuu kwa kudanganyika kuwa kuna mafuta yatakayochimbwa kwa siku mia moja na kueleza kuwa anauhakika na anaamini kuwa Dk. Shein atapandisha tena bei zao la karafuu baada ya kuchaguliwa tena kuwa Rais wa Zanzibar.

Nao viongozi wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba chini ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo Hamad Mberwa walipongeza juhuddi zinazochukuliwa na viongozi wa CCM katika kuimarisha chama hicho huko katika Mkoa wa Kaskaziani Pemba.

Aidha, viongozi hao walitumia futrsa hiyo kuwaeleza historia ya Mtambwe ilivyokuwa hapo kabla na hivi sasa ilivyo kwani maendeleo makubwa yamepatikanwa huko Mtambwe.

Katibu wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba,   alisema kuwa Mtambwe ya sasa ni Mtambwe ya Dijitali na sio ile iliyozoeleka kwani tayari wameshatambua ukweli uko wapi na chama kipi cha kukiunga mkono ili kiwaletee maendeleo.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
 

0 comments:

Post a Comment

 
Support by Tone multimedia company Limited
Copyright © 2012. Zanzibar Yetu - All Rights Reserved
Designed by by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa